WENYEJI, Azam FC wameibuka na ushindi wa 4-1 dhidi ya JKU ya Zanzibar katika mchezo wa kirafiki jioni ya leo Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam.
Mabao ya Azam FC leo yamefungwa na Mkongo Idris Mbombo moja kwa penalti dakika ya 19 na lingine dakika ya 40 na Wazambia, Charles Zulu dakika ya 23 na Rodgers Kola dakika ya 90, wakati la JKU limefungwa na Mustafa Hassan dakika ya 81 kwa penalti pia.
0 comments:
Post a Comment