• HABARI MPYA

    Monday, November 22, 2021

    TANZANIA YAMALIZA YA PILI COSAFA


    TANZANIA jana imemaliza nafasi ya pili kwenye michuano ya Soka la Ufukweni baada ya kufungwa 3-1 na Msumbiji katika Fainali ufukwe wa South Beach Arena Jijini Durban.
    Ushindi huo ni mwendelezo wa ubabe wa Msumbiji kwa Tanzania, kwani mechi ya Kundi B walishinda kwa penalti 4-3 baada ya sare ya 4-4.
    Mechi nyingine Tanzania iliyo chini ya kocha Boniphace Pawasa ilishinda 3-1 dhidi ya Comoro Kundi A kabla ya kuifunga Angola 5-2 kwenye Nusu Fainali.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: TANZANIA YAMALIZA YA PILI COSAFA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top