Na Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM
KLABU ya Simba kesho inatarajiwa kufanya Semina kubwa ya Wanachama wote wa klabu hiyo kuwapa elimu ya mabadiliko.
Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa klabu ya Simba, Haji Manara amesema kwamba semina hiyo inalenga kujenga uelewa mpana zaidi juu ya muundo mpya wa uendeshwaji wa klabu hiyo.
Manara amesema na hiyo inafuatia mabadiliko ya Katiba ya Simba yaliyofanywa na wanachama wa klabu hiyo na kusajiliwa na Msajili wa Vyama vya Michezo na Klabu nchini.
“Maandalizi yote ya Semina hiyo yamekamilika,na itafanyika kesho tarehe 16 mwezi wa 8 mwaka 2017, ambayo itakuwa ni Jumatano kuanzia Saa Nane na Nusu mchana (8.30)”.
Manara amesema Semina hiyo itafanyikia kwenye ukumbi wa Mikumi uliopo kwenye eneo la maonyesho ya kimataifa ya biashara ya Sabasaba (PTA), Kurasini mjini Dar es Salaam.
“Tunawaomba wanachama wote popote walipo waje kwa wingi hapo kesho, huku klabu ikiwaomba viongozi wa Simba Wilaya ya Temeke waandae utaratibu mzuri wa kuwapokea wageni,” amesema.
KLABU ya Simba kesho inatarajiwa kufanya Semina kubwa ya Wanachama wote wa klabu hiyo kuwapa elimu ya mabadiliko.
Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa klabu ya Simba, Haji Manara amesema kwamba semina hiyo inalenga kujenga uelewa mpana zaidi juu ya muundo mpya wa uendeshwaji wa klabu hiyo.
Manara amesema na hiyo inafuatia mabadiliko ya Katiba ya Simba yaliyofanywa na wanachama wa klabu hiyo na kusajiliwa na Msajili wa Vyama vya Michezo na Klabu nchini.
“Maandalizi yote ya Semina hiyo yamekamilika,na itafanyika kesho tarehe 16 mwezi wa 8 mwaka 2017, ambayo itakuwa ni Jumatano kuanzia Saa Nane na Nusu mchana (8.30)”.
Manara amesema Semina hiyo itafanyikia kwenye ukumbi wa Mikumi uliopo kwenye eneo la maonyesho ya kimataifa ya biashara ya Sabasaba (PTA), Kurasini mjini Dar es Salaam.
“Tunawaomba wanachama wote popote walipo waje kwa wingi hapo kesho, huku klabu ikiwaomba viongozi wa Simba Wilaya ya Temeke waandae utaratibu mzuri wa kuwapokea wageni,” amesema.
0 comments:
Post a Comment