• HABARI MPYA

    Tuesday, March 24, 2015

    YANGA SC NA JKT RUVU KESHO TAIFA

    Na Baraka Kizuguto, DAR ES SALAAM 
    LIGI Kuu ya Vodacom Tanzania Bara ianatrajiwa kuendelea kesho (jumatano) kwa mchezo mmoja kupigwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam, kwa wenyeji JKT Ruvu kuwakaribisha vinara wa ligi hiyo timu ya Yanga SC.
    Yanga SC itahitaji ushindi katika mchezo huo, ili kuzidi kupiga kasi katika marathoni ya ubingwa wa Ligi Kuu.
    Hadi sasa, ikiwa na pointi 37 baada ya kucheza mechi 18, Yanga SC ipo kileleni mwa Ligi Kuu, ikifuatiwa na mabingwa watetezi, Azam FC wenye pointi 36 za mechi 18 pia.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: YANGA SC NA JKT RUVU KESHO TAIFA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top