// Disable text selection (not fully reliable) function disableSelection(element) { element.setAttribute('unselectable', 'on'); element.style.userSelect = 'none'; element.style.MozUserSelect = 'none'; element.style.webkitUserSelect = 'none'; } // Apply to the entire document body document.addEventListener('DOMContentLoaded', function() { disableSelection(document.body); }); MUHAMMAD ALI ATOKA HOSPITALI, ASHEREHEKEA MIAKA 73 YA KUZALIWA LEO - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE MUHAMMAD ALI ATOKA HOSPITALI, ASHEREHEKEA MIAKA 73 YA KUZALIWA LEO - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE
  • HABARI MPYA

    Saturday, January 17, 2015

    MUHAMMAD ALI ATOKA HOSPITALI, ASHEREHEKEA MIAKA 73 YA KUZALIWA LEO

    GWIJI wa masumbwi duniani, Muhammad Ali ameruhusiwa kutoka hospitali nchini Marekani ambako alikuw amelazwa kwa matibabu ya kibofu cha mkojo na leo atasherehekea kuzaliwa kwake pamoja na familia.
    Hii ilikuwa ni mara ya pili kwa bondia huyo kulazwa hospitali katika wiki nne zilizopita.
    Msemaji wa familia ya Ali, Bob Gunnell amesema aliondoka katika hospitali ambayo haikutajwa na kurejea katika moja ya nyumba zake. 
     Muhammad Ali has been released from hospital after treatment for a urinary tract infection
    Muhammad Ali ameruhusiwa kutoka hospitali baada ya matibabu ya kibofu cha mkojo
    Ali, standing over Sonny Liston in 1965,  is generally regarded as the greatest heavyweight boxer of all time
    Ali, akiwa amesimama baada ya kumbwaga chini Sonny Liston mwaka 1965,  anapewa heshima ya bondia bora wa uzito wa juu daima

    Gunnell amesema Ali anatarajiwa kusherehekea miaka ya 73 ya kuzaliwa kwake na familia pamoja marafiki na jamaa mbalimbali.Bingwa huyo wa ndondi za uzito wa juu wa zamani duniani na mkewe, Lonnie, wana nyumba Arizona, Michigan na nyumbani kwao, Louisville.
    Ali alipeleka hospitali mwishoni mwa mwezi uliopita kwa maradhi ambayo awali ilidhaniwa ni Nimonia. Baadaye madaktari wakagundua Ali anasumbuliwa na matatizo ya kibofu cha mkojo na si Nimonia.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MUHAMMAD ALI ATOKA HOSPITALI, ASHEREHEKEA MIAKA 73 YA KUZALIWA LEO Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top