// Disable text selection (not fully reliable) function disableSelection(element) { element.setAttribute('unselectable', 'on'); element.style.userSelect = 'none'; element.style.MozUserSelect = 'none'; element.style.webkitUserSelect = 'none'; } // Apply to the entire document body document.addEventListener('DOMContentLoaded', function() { disableSelection(document.body); }); ETO'O AREJEA ITALIA - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE ETO'O AREJEA ITALIA - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE
  • HABARI MPYA

    Saturday, January 17, 2015

    ETO'O AREJEA ITALIA

    MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Cameroon, Samuel Eto'o amekubali kujiunga na Sampdoria baada ya klabu hiyo ya Italia kufikia makubaliano na wakala wake.
    Mkongwe huyo mwenye umri wa miaka 33 anayechezea Everton kwa sasa, amepewa ofa ya Mkataba wa miaka miwili na nusu na uwezekano wa kuwa kocha atakapostaafu soka.
    Familia ya Eto'o bado inaishi mjini Milan na alikuwa anataka kurejea Italia.
    Striker Samuel Eto'o appears to be set to leave Everton for a return to Italy with Sampdoria
    Mshambuliaji Samuel Eto'o anajiandaa kuondoka Everton arejee Italia kujiunga na Sampdoria

    Sampdoria inataka asafiri kwenda Genoa kesho tayari kwa vipimo vya afya Jumatatu kisha awekwe kwenye kikosi kitakachomenyana na klabu yake ya zamani, Inter Milan katika Kombe la Italia Jumatano.
    Everton bado wanatafakari vipengele vya Mkataba wa uhamisho kabla ya hawajamkubalia kuondoka.
    Kikosi cha Roberto Martinez kitamenyana na West Bromwich Albion Uwanja wa Goodison Park Jumatatu katika Ligi Kuu ya England. 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: ETO'O AREJEA ITALIA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top