// Disable text selection (not fully reliable) function disableSelection(element) { element.setAttribute('unselectable', 'on'); element.style.userSelect = 'none'; element.style.MozUserSelect = 'none'; element.style.webkitUserSelect = 'none'; } // Apply to the entire document body document.addEventListener('DOMContentLoaded', function() { disableSelection(document.body); }); MESSI AIPA USHINDI BARCELONA DHIDI YA ATLETICO MADIRD - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE MESSI AIPA USHINDI BARCELONA DHIDI YA ATLETICO MADIRD - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE
  • HABARI MPYA

    Thursday, January 22, 2015

    MESSI AIPA USHINDI BARCELONA DHIDI YA ATLETICO MADIRD

    BAO pekee la Lionel Messi limeipa ushindi mwembamba wa 1-0 nyumbani, Uwanja wa Camp Nou, Barcelona dhidi ya Atletico Madrid katika Robo Fainali ya kwanza ya Kombe la Mfalme Hispania.
    Messi alifunga bao hilo dakika ya 85 usiku wa kuamkia leo, baada ya kuuwahi mpira uliookolewa na Jan Oblak kufuatia mkwaju wa penalti alioupiga yeye mwenyewe na kuutumbukiza nyavuni.
    Penalti hiyo ilitolewa baada ya Juanfran kumchezea rafu Sergio Busquets na sasa timu hizo zitarudiana wiki ijayo katika Robo Fainali ya pili ya michuano hiyo Uwanja wa Vicente Calderon. Fernando Torres alianza jana katika kikosi cha Atletico, lakini akatolewa mapumziko kumpisha Mario Mandzukic.
    Lionel Messi (left) runs off in celebration after scoring the rebound having missed a penalty to put Barcelona ahead against Atletico Madrid
    Lionel Messi (kushoto) akikimbia kushangilia na Luis Suarez baada ya kuifungia bao pekee Barcelona dhidi ya Atletico Madrid

    PICHA ZAIDI NENDA: http://www.dailymail.co.uk/sport/football/article-2920515/Barcelona-1-0-Atletico-Madrid-Lionel-Messi-misses-penalty-scores-rebound.html#ixzz3PWDrlzEc 

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MESSI AIPA USHINDI BARCELONA DHIDI YA ATLETICO MADIRD Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top