Kocha wa Yanga SC, Mholanzi Hans van der Pluijm (kulia) akipeana mikono na shabiki na mwanachama wa klabu hiyo, maarufu kama Carlos jana Uwanja wa Amaan, Zanzibar wakati Simba SC ikimenyana na Taifa ya Jang'ombe katika Robo Fainali ya Kombe la Mapinduzi. Carlos alilala rumande juzi baada ya kuingia uwanjani na kwenda kuchukua glavu za akiba za kipa wa Shaba, Bakari Shaweji katika mchezo wa mwisho wa Kundi A, akidhani ni uchawi uliokuwa ukisababisha wachezaji wa timu yao wakose mabao ya wazi. Dakika tano baada ya Carlos kutoa glavu hizo, Yanga ilipata bao dakika ya 86 lililofungwa na Andrey Coutinho na Carlos akapewa sifa ya kusababisha bao hilo pekee katika ushindi wa 1-0. |
0 comments:
Post a Comment