// Disable text selection (not fully reliable) function disableSelection(element) { element.setAttribute('unselectable', 'on'); element.style.userSelect = 'none'; element.style.MozUserSelect = 'none'; element.style.webkitUserSelect = 'none'; } // Apply to the entire document body document.addEventListener('DOMContentLoaded', function() { disableSelection(document.body); }); KIIZA ATUA FANJA YA OMAN - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE KIIZA ATUA FANJA YA OMAN - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE
  • HABARI MPYA

    Thursday, January 01, 2015

    KIIZA ATUA FANJA YA OMAN

    Na Prince Akbar, DAR ES SALAAM
    ALIYEKUWA mshambuliaji wa Yanga SC, Hamisi Kiiza ‘Diego’ atajiunga na Fanja SC ya Oman, imefahamika.
    Wakala wa wachezaji, Said Maaskary anayetambuliwa na Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA), ameiambia BIN ZUBEIRY jana kwa simu kutoka Oman, kwamba Fanja imekwishamalizana na Kiiza na anakwenda Muscat kusaini Mkataba.
    Maaskary amesema Kiiza atafika Muscat Ijumaa kusaini Mkataba na mara moja kuanza maisha mapya bara la Asia.
    Kiiza alitemwa Yanga SC katika dirisha dogo kumpisha mshambuliaji Mliberia, Kpah Sherman na awali alijaribu kwenda Mnyamar ambako hata hivyo hakufanikiwa.
    Hamisi Kiiza kushoto anakwenda kuanza maisha mapya Oman

    Kiiza aliichezea Yanga SC tangu mwaka 2012 akitokea Bunamwaya ya kwao, Uganda na katika kipindi chote hicho alikuwa tegemeo la mabao la timu hiyo.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: KIIZA ATUA FANJA YA OMAN Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top