WENYEJI Brazil, wamelazimishwa safe ya bila kufungana na Mexico katika mchezo wa Kundi A Kombe la Dunia uliomalizika muda mfupi uliopita.
Brazil wakiongozwa na nyota wake, Neymar walicheza vizuri na kushambulia mno langoni mwa wapinzani wao hao wa Amerika Kusini pia, lakini wakakosa bahati ya kufunga.
Timu hiyo inayofundishwa Luiz Felipe Scolari ilifanya jitihada nyingi za kufunga kwa kutengeneza nafasi nyingi, lakini sifa zimuendee kipa wa Mexico, Guillermo Ochoa, aliyeinusuru timu yake kwa kuokoa mabao mawili au matatu ya wazi mno.
Ulinzi mkali: Neymar akijaribu kuwatoka mabeki wa Mexico katika mchezo ulioisha kwa sare ya bila kufungana
Sare hiyo inaiacha Brazil iendelee kuishi kileleni mwa kundi hilo baada ya kufikisha pointi nne, baada ya awali kuifunga Croatia 3-1.
Kikosi cha Brazil kilikuwa: Julio Cesar, Dani Alves, Thiago Silva, Luiz, Marcelo, Paulinho, Gustavo, Ramires/Bernard dk45, Oscar/Willian dk84, Neymar na Fred/Jo dk68.
Mexico: Ochoa, Aguilar, Rodriguez, Marquez, Moreno, Layun, Herrera/Fabian dk76, Vazquez, Guardado, Giovani/Jiminez dk84, Peralta/Hernandez dk74.
Bao la wazi: Neymar aliruka hewani kupiga kichwa vizuri akimzidi Rafael Marquez
Lakini kips wa Mexico, Guillermo Ochoa akaokoa
Neymar akimroka Andres Guardado



.png)
0 comments:
Post a Comment