• HABARI MPYA

    Monday, March 31, 2014

    TIMU YA OKWI, ETOILE YAPETA AFRIKA

    ETOILE du Sahel ya Tunisia imeitoa SuperSport United ya Afrika Kusini kwa jumla ya mabao 5-1 katika Kombe la Shirikisho Afrika baada ya juzi kuilaza mabao 4-1 Afrika Kusini.
    Timu hiyo ya zamani ya mshambuliaji wa Yanga SC, Emmanuel Okwi katika mchezo wa kwanza ilishinda bao 1-0 na sasa inakwenda Hatua ya 16 Bora ambako itamenyana na moja ya timu zilizotolewa katika Ligi ya Mabingwa kupata tiketi ya kucheza Hatua ya Makundi.

    Katika mechi nyingine za juzi, Bayelsa United ya Nigeria iliitoa How Mine ya Zumbabwe kwa jumla ya mabao 3-2, ikianza kufungwa 2-1 ugenini na Jumamosi kushinda 2-0 nyumbani, Difaa El Jadida ya Morocco imeitoa AS Kigali kwa jumla ya mabao 3-1 ikishinda 3-0 juzi baada ya kufungwa 1-0 katika mchezo wa kwanza.
    Katika mechi za jana, ASEC Mimosas ya Ivory Coast iliifumua CS Constantine ya Algeria mabao 6-0, Petro Atletico ya Angola iliifunga 1-0 Ismailia ya Misri baada ya sare 0-0 katika mchezo wa kwanza. 
    Djoliba ya Mali ilisonga mbele kwa ushindi wa penalti 3-2 baada ya sare ya jumla ya 2-2 na Wadi Degla ya Misri kila timu ikishinda 2-0 nyumbani kwake, CA Bizertin ya Tunisia iliifunga 2-1 Warri Wolves ya Nigeria baada ya sare ya 0-0 katika mchezo wa kwanza na Zesco United ya Zambia imeifunga 1-0 Medeama ya Ghana baada ya kufungwa 2-0 katika mchezo wa kwanza, hivyo imeaga.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: TIMU YA OKWI, ETOILE YAPETA AFRIKA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top