• HABARI MPYA

    Tuesday, March 25, 2014

    KAMATI YA SHERIA KUPITIA MAREKEBISHO YA KATIBA

    Na Boniface Wambura, Dar es Salaam
    KAMATI ya Sheria na Hadhi za Wachezaji ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) inatarajia kukutana mwishoni mwa wiki kupitia taarifa ya utekelezaji wa agizo la wanachama kurekebisha katiba zao.
    TFF ilitoa agizo kwa wanachama wetu kufanyia marekebisho katiba ikiwemo kuingiza Kamati ya Maadili. Mwisho wa utekelezaji wa agizo hilo ulikuwa Machi 20 mwaka huu.
    Rais wa TFF, Jamal Malinzi kushoto akiwa na Rais wa CAF, Issa Hayatou kulia

    Hivyo, Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji itapokea taarifa ya utekelezaji wa agizo hilo kutoka kwa Sekretarieti, na baadaye kutoa mwongozo wa hatua inayofuata.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: KAMATI YA SHERIA KUPITIA MAREKEBISHO YA KATIBA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top