• HABARI MPYA

    Tuesday, February 21, 2012

    PRINCE NASEEM ULINGONI MBAGALA

    BINGWA wa mkanda wa Shirikisho la ngumi za kulipwa Tanzania (PST)
    Abdalah Mohamed 'Prenc Naseem' atapanda ulingoni kutetea mkanda wake
    wa PST Februari 24 mwaka huu dhidi ya Salehe Mkalekwa.
    Pambano hilo la ubingwa wa PST litakuwa ni pambano la uzito wa kg 57
    na litashirikisha mapambano mengine manne ya utangulizi.
    Akizungumza Dar es Salaam jana, Mratibu wa pambano hilo Shaban Adiosi
    'Mwayamwaya' alisema pambano hilo litafanyika katika ukumbi wa New
    Kibeta uliopo mbagala kuu Dar es Salaam.
    Alisema pambano hilo la ubingwa wa PST ni muendelezo wa shirikisho
    hilo kuendelea kuinua mabondia ambao hawajawa na majina
    makubwa ili nao waweze kufikia kiwango kizuri cha mchezo huo.
    "Ubingwa huu wa PST ni maalum kwa ajili ya mabondia chipkizi na ndio
    maana mabondia wanaoshirikishwa wengi ni chipkizi na lengo ni
    kuendeleza vipaji vyao,"alisema Mwayamwaya.
    Aliyataja mapambano ya utangulizi yatakayopamba pambano hilo yatakuwa
    kati ya Shaaban Zungu na Hasan Debe watakaopigana uzito wa kg 55,
    Safari Mbeyu na Ibrahim Maokola watakaopigana uzito wa kg 67, Jofrey
    Pacho atakayetwangana na Dickson Kawiani na Kulwa Kindondi
    atakayepigana na Khaji Hamisi.
    Mbali na kuwepo mapambano ya ngumi kutakuwa na uuzwaji wa DVD zenye
    mapambano ya mabingwa wa Dunia akiwemo Manny Paquaio, Floyd Maywherth,
    Roy Jones, Lenox Lewis,David Haye na wengine kibao ‘DVD’ hizo zilizoandaliwa kwa ubora wa hali
    ya juu zitakuwa zikiuzwa kwenye mpambano huo na Kocha wa Kimataifa wa Mchezo wa Ngumi, Rajabu Mhamila
    ‘Super ‘D’.
    “Ninatarajia kuwapelekea DVD mashabiki wa ngumi watakaokuwepo katika
    pambano kujifunza mambo mbalimbali ikiwa ni pamoja na sheria za mchezo
    wa ngumi,” alisema Super ‘D’.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: PRINCE NASEEM ULINGONI MBAGALA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top