KLABU
ya Chelsea italazimika kucheza tena na Birmingham katika Raundi ya tano ya
Kombe la FA, baada ya leo kulazimishwa sare ya kufungana bao 1-1 na timu hiyo
ya Daraja la Kwanza, hivyo kuzidi kumuweka katika wakati mgumu kocha Andre
Villas-Boas.
Birmingham
ilimpoteza Nahodha wake, Stephen Carr dakika ya 12 aliyeumia, lakini
walifanikiwa kupata bao la kuongoza kwenye Uwanja wa Stamford Bridge dakika
nane baadaye kupitia kwa David Murphy.
Chelsea
ilipata penalti dakika ya 22, wakati Wade Elliott alipomchezea rafu Ramires,
lakini kipa Colin Doyle aliokoa mkwaju wa Juan Mata.
Chelsea
ililazimika kusubiri hadi dakika ya 62 kupata bao la kusawazisha kupitia kwa Daniel
Sturridge.
Vyombo
vya habari England kwa kiasi kikubwa vimekuwa vikiripoti kiwamba, kocha Villas-Boas
ametofautiana na wachezaji kibao wa timu hiyo wanaopinga mbinu zake za
ufundishaji.


.png)
0 comments:
Post a Comment