• HABARI MPYA

    Sunday, February 19, 2012

    DINHO BADO NOMA KWA MABAO, AITAKATISHA FLAMENGO

    MWANASOKA bora wa zamani wa dunia, Ronaldinho na Vagner Love walifunga mabao kipindi cha pili na kuisaidia Flamengo kutoka nyuma na kuibuka na ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Resende jana katika Nusu Fainali ya Guanabara Cup, hatua ya kwanza ya Rio championship. Vasco da Gama, Botafogo na Fluminense pia zimeingia Nusu Fainali.
    Flamengo ilitanguliwa wakati Marcelo Regis alipoifungia Resende dakika ya 47, lakini Ronaldinho na mshambuliaji wa zamani wa CSKA Moscow, Vagner Love wakaifungia klabu hiyo maarufu zaidi Brazil dakika 10 baadaye, wakipishana dakika tano tano.
    Ronaldinho alisawazisha kwa kichwa dakika ya 57 na Vagner Love aliyesajiliwa hivi karibuni, akapiga la pili dakika ya 62. Mshambuliaji Negueba alihitimisha ushindi kwa bao lake dakika ya 72.
    Matokeo hayo yatawakutanisha na na Vasco da Gama katika Nusu Fainali, ambayo iliifunga Boavista 1-0.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: DINHO BADO NOMA KWA MABAO, AITAKATISHA FLAMENGO Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top