// Disable text selection (not fully reliable) function disableSelection(element) { element.setAttribute('unselectable', 'on'); element.style.userSelect = 'none'; element.style.MozUserSelect = 'none'; element.style.webkitUserSelect = 'none'; } // Apply to the entire document body document.addEventListener('DOMContentLoaded', function() { disableSelection(document.body); }); LAMPARD AING'ARISHA MAN CITY - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE LAMPARD AING'ARISHA MAN CITY - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE
  • HABARI MPYA

    Thursday, January 01, 2015

    LAMPARD AING'ARISHA MAN CITY

    TIMU ya Manchester City imeifikia kwa pointi Chelsea kileleni mwa Ligi Kuu ya England, kufuatia ushindi wa mabao 3-2 dhidi ya Sunderland Uwanja wa Etihad.
    Shukrani kwake, kiungo mkongwe Frank Lampard aliyeifungia City bao la ushindi dakika ya 73 kwa kichwa akimalizia krosi ya Gael Clichy na timu hiyo inatimiza pointi 46 na mechi moja zaidi ya The Blues, 20.
    Baada ya kipindi cha kwanza kibovu, City iliingia na moto kipindi cha pili wakati Yaya Toure alipoifungia bao la kwanza nje ya boksi dakika ya 56, kabla ya Stevan Jovetic kufunga la pili dakika ya 66.
    Sunderland ikafanikiwa kusawazisha mabao yote akianza Jack Rodwell dakika ya 68 akiifunga klabu yake ya zamani na Adam Johnson kwa penalty dakika ya 72 baada ya Pablo Zabaleta kumchezea rafu Billy Jones. 
    Frank Lampard gives the thumbs up after scoring Man City's third goal as Sunderland goalkeeper Costel Pantilimon stands dejected
    Frank Lampard akionyesha dole gumba baada ya kuifungia Man City bao la ushindi

    PICHA ZAIDI NENDA: http://www.dailymail.co.uk/sport/football/article-2893373/Manchester-City-3-2-Sunderland-Frank-Lampard-scores-winner-settle-thrilling-contest-Manuel-Pellegrini-s-men-draw-level-points-Chelsea-Premier-League.html#ixzz3NaudrYSf 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: LAMPARD AING'ARISHA MAN CITY Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top