// Disable text selection (not fully reliable) function disableSelection(element) { element.setAttribute('unselectable', 'on'); element.style.userSelect = 'none'; element.style.MozUserSelect = 'none'; element.style.webkitUserSelect = 'none'; } // Apply to the entire document body document.addEventListener('DOMContentLoaded', function() { disableSelection(document.body); }); BOCCO MCHEZAJI WA KWANZA KUPEWA ‘THANK YOU’ SIMBA SC - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE BOCCO MCHEZAJI WA KWANZA KUPEWA ‘THANK YOU’ SIMBA SC - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE
  • HABARI MPYA

    Monday, June 17, 2024

    BOCCO MCHEZAJI WA KWANZA KUPEWA ‘THANK YOU’ SIMBA SC

    MSHAMBULIAJI na aliyekuwa Nahodha wa timu kwa mafanikio kwa misimu kadhaa, John Raphael Bocco amekuwa mchezaji wa kwanza kuachwa Simba SC.
    Bocco (34) aliyejiunga na Simba SC mwaka 2017 akitokea Azam FC alicheza nusu ya kwanza tu ya msimu uliomalizika, kabla ya kuumia kwenye michuano ya Kombe la Mapinduzi visiwani Zanzibar. 
    Alilikuwa sehemu ya wachezaji wa akiba kwenye mechi ya kwanza ya Mapinduzi dhidi ya JKU Januari 1 mwaka huu Simba SC ikishinda 3-1 na akapangwa aanze mechi ya pili, bahati mbaya akaumia katika mazoezi ya kupasha misuli moto Januari 3 dhidi ya Singida Fountain Gate na ndio akamaliza msimu.
    Simba ilishinda 2-0 mechi hiyo ya Kundi B na kwenda Robo Fainali na wakafika hadi Fainali wakafungwa 1-0 na Mlandege Uwanja wa New Amaan Complex, Zanzibar.
    Tangu aumie Bocco amepewa jukumu la kufundisha kikosi cha timu ya vijana cha Simba chini ya umri wa miaka 17.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: BOCCO MCHEZAJI WA KWANZA KUPEWA ‘THANK YOU’ SIMBA SC Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top