// Disable text selection (not fully reliable) function disableSelection(element) { element.setAttribute('unselectable', 'on'); element.style.userSelect = 'none'; element.style.MozUserSelect = 'none'; element.style.webkitUserSelect = 'none'; } // Apply to the entire document body document.addEventListener('DOMContentLoaded', function() { disableSelection(document.body); }); MANYIKA KIPA BORA, HAJIBU UFUNGAJI BORA NA NDEMLA UCHEZAJI BORA KOMBE LA MAPINDUZI - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE MANYIKA KIPA BORA, HAJIBU UFUNGAJI BORA NA NDEMLA UCHEZAJI BORA KOMBE LA MAPINDUZI - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE
  • HABARI MPYA

    Monday, January 12, 2015

    MANYIKA KIPA BORA, HAJIBU UFUNGAJI BORA NA NDEMLA UCHEZAJI BORA KOMBE LA MAPINDUZI

    Na Mahmoud Zubeiry, ZANZIBAR
    WAKATI michuano ya Kombe la Mapinduzi inafikia tamati kesho, mshambuliaji wa Simba SC Ibrahim Salum Hajibu yupo katika nafasi nzuri ya kuwa mfungaji bora, huku Peter Manyika akiwania kuwa kipa bora.Kwa sasa, Hajibu anashika nafasi ya pili kwa kufunga mabao katika mashindano haya ya takriban wiki mbili kwa mabao yake matatu aliyofunga katika mchezo mmoja dhidi ya Taifa Jang’ombe, Simba SC ikishinda 4-0 na kwenda Nusu Fainali.
    Anayeongoza kwa mabao ni Simon Msuva aliyefunga mara nne, lakini kwa bahati mbaya, timu yake Yanga SC ilitolewa katika Robo Fainali na JKU.
    Ibrahim Hajibu wa pili kulia baada ya Said Ndemla, anaweza kuibuka mfungaji bora wa Kombe la Mapinduzi mwaka huu iwapo atafunga kesho

    VINARA WA MABAO KOMBE LA MAPINDUZI

    Simon Msuva   Yanga 4
    Andy Coutinho Yanga
    Ibrahim Hajibu  Simba 3  
    William Wadri    KCCA 3        
    Amour Omary   JKU 3
    Kpah Sherman  Yanga 2       
    Rama Singano  Simba 2
    Mbrazil Andrey Coutinho wa Yanga SC pia, Mganda William Wadri wa KCCA na Amour Omar ‘Janja’ wa JKU nao wana mabao matatu kila mmoja sawa na Hajibu, lakini wote wamekwishaaga mashindano baada ya timu zao kutolewa.
    Mchezaji mwenye nafasi ya kumpiku Hajibu, ni winga wa Simba SC, Ramadhani Singano ‘Messi’ mwenye mabao mawili sawa Mliberia Kpah Sherman wa Yanga SC.
    Messi aliyefunga bao pekee katika ushindi wa 1-0 katika Nusu Fainali Simba SC ikiifunga JKU, anatarajiwa kuanza kesho katika kikosi cha kwanza, wakati Hajibu anaweza kuendelea kutokea benchi.
    Mashindano ya Kombe la Mapinduzi yanaonekana kumuibua tena Messi, ambaye siku za karibuni cheche zake ziliyeyuka.
    Aidha, kipa mdogo Peter Manyika amejiweka katika mazingira mazuri ya kushinda tuzo ya mlinda mlango bora, baada ya kudaka mechi nne mfululizo bila kufungwa hata bao moja.
    Peter Manyika anaweza kuwa kipa bora
    Mtoto huyo wa kipa wa zamani wa kimataifa Tanzania na klabu ya Yanga SC, alifungwa bao moja katika mchezo wa kwanza na Mtibwa Sugar Simba SC ikilala 1-0, lakini baadaye akadaka Wekundu wa Msimbazi wakishinda 1-0 mara tatu dhidi ya Mafunzo, JKU mara mbili mchezo wa Kundi C na Nusu Fainali na 4-0 dhidi ya Taifa.  
    Mpinzani wa Manyika katika tuzo ya kipa bora, ni Said Mohammed wa Mtibwa Sugar ambaye amefungwa bao moja na pia aliokoa penalti mara mbili katika Robo Faiali na Nusu Fainali, akiiwezesha timu yake kufika Fainali. 
    Kiungo Said Ndemla wa Simba SC, beki Salum Mbonde wa Mtibwa Sugar, wote wamecheza vizuri mechi zote za timu zao hadi sasa na haitakuwa ajabu mmoja kati yao, akitajwa mchezaji biora wa mashindano, iwapo atarudia kucheza vizuri kesho Uwanja wa Amaan usiku katika Fainali.

    ORODHA YA MABINGWA KOMBE LA MAPINDUZI

    Mwaka   Bingwa Mshindi wa Pili
    2007 Yanga SC  Mtibwa Sugar 
    2008 Simba SC  Mtibwa Sugar
    2009 Miembeni        KMKM
    2010 Mtibwa Sugar Ocean View
    2011 Simba SC   Yanga SC
    2012 Azam FC  Simba SC
    2013 Azam FC  Tusker FC
    2014 KCCA        Simba SC
    2015 ??????? ???????
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MANYIKA KIPA BORA, HAJIBU UFUNGAJI BORA NA NDEMLA UCHEZAJI BORA KOMBE LA MAPINDUZI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top