• HABARI MPYA

    Sunday, March 17, 2013

    MECHI YA RUVU SHOOTING, YANGA YAINGIZA MIL 62/-

    Mfungaji wa bao pekee la ushindi la Yanga jana, Hamisi Kiiza kulia akimtoka beki wa Ruvu Shooting

    Na Boniface Wambura
    MECHI ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, kati ya Ruvu Shooting na Yanga iliyochezwa jana Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam imeingiza sh. 62,228,000 kutokana na watazamaji 10,929.
    Viingilio katika mechi hiyo namba 146 iliyomalizika kwa Yanga kuibuka na ushindi wa bao 1-0 vilikuwa sh. 5,000, sh. 8,000, sh. 15,000 na sh. 20,000 huku kila klabu ikipata mgawo wa sh. 14,336,764.95 wakati Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) iliyolipwa ni sh. 9,492,406.78.
    Mgawo mwingine wa mapato hayo ni asilimia 15 ya uwanja sh. 7,289,880.48, tiketi sh. 4,136,390, gharama za mechi sh. 4,373,928.29, Kamati ya Ligi sh. 4,373,928.29, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 2,186,964.14, Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Pwani (COREFA) sh. 850,486.06 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 850,486.06.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: MECHI YA RUVU SHOOTING, YANGA YAINGIZA MIL 62/- Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top