Pierre-Emerick Aubameyang akishangilia baada ya kuifungia bao pekee Arsenal dakika ya 10 ikiwalaza wenyeji, Watford 1-0 katika mchezo wa Ligi Kuu ya England Uwanja wa Vicarage Road huku akimaliza ukame wake wa mabao wa mechi saba. Watford ilimaliza pungufu baada ya Troy Deeney kutolewa kwa kadi nyekundu ya moja kwa moja kwa kosa la kumpita Lucas Torreira dakika ya 11 tu na kwa ushindi huo, Arsenal inafikisha pointi 66 sawa na Chelsea katika mchezo wa 33 na kurejea nafasi ya nne ikiizidi kwa pointi mbili Manchester United inayoshika nafasi ya sita PICHA ZAIDI GONGA HAPA
How emotive tifo gave Palace fans belief of cup final win
-
A tifo displayed by Crystal Palace fans paid tribute to lost loved ones
during their historic 1-0 win over Manchester City in Saturday's FA Cup
final.
41 minutes ago
0 comments:
Post a Comment