Washambuliaji Luis Suarez (kulia) na Lionel Messi (kushoto) wakipongezana baada ya wote kufunga katika ushindi wa 2-1 wa Barcelona dhidi ya Atletico Madrid usiku wa jana kwenye Nusu Fainali ya kwanza ya Kombe la Mfalme Uwanja wa Vicente Calderon mjini Madrid, Hispania. Suarez alifunga dakika ya saba akimalizia pasi ya Javier Mascherano na Messi dakika ya 33 akimalizia pasi ya Ivan Rakitic, kabla Antoine Griezmann kuifungia Atletico dakika ya 59 akimalizia pasi ya Diego Godin. Barcelona sasa watakuwa wenyeji wa Atletico Madrid katika mchezo wa marudiano Jumanne Uwanja wa Nou Camp PICHA ZAIDI GONGA HAPA
Chelsea's Palmer and Pedro feature in Madonna video
-
Chelsea forwards Cole Palmer and Joao Pedro make a surprise appearance in a
promotional film for Madonna's new album.
7 minutes ago



.png)
0 comments:
Post a Comment