• HABARI MPYA

    Wednesday, November 13, 2013

    KILI MARATHON 2014 YAZINDULIWA LEO, ZAWADI SI MCHEZO

    Na Ibrahim Kyaruzi, Dar es Salaam
    MASHINDANO ya 12 ya mbio za Kilimanjaro Marathon yanayotarajiwa kufanyika mjini Moshi mkoani Kilimanjaro Machi 2, mwakani yamezinduliwa jijini Dar es Salaam leo.
    Katika uzinduzi huo, Meneja wa Bia ya Kilimanjaro, George Kavishe alisema: “Ninayo furaha kutangaza kwamba huu utakuwa mwaka wa 12 kwa mbio za Kilimanjaro Marathon kufanyika chini ya udhamini wa Kilimanjaro Premium Lager.
    Mgeni rasmi, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari Utamaduni na Michezo, Elisante Ole Gabriel akimkabidhi bendera ya mbio za Kilimanjaro Marathon, Katibu wa Chama cha Riadha Tanzania (RT), Selemani Nyambui wakati wa hafla ya uzinduzi wa mbio hizo asubuhi ya leo kwenye ukumbi wa Serengeti katika hoteli ya JB Bellomonte, jengo la Benjamin Mkapa, Dar es Salaam. Wengine katikati ni Meneja Uhusiano wa Vodacom Tanzania, Salum Mwalimu kushoto na Meneja wa Bia ya Kilimanjaro, George Kavishe.  
    Kwa mara nyingine, ni fahari kubwa kwa Kilimanjaro Premium Lager kudhamini tukio hili maarufu na lenye msisimko mkubwa katika kalenda ya michezo ya Tanzania.”
    Kavishe alitangaza nyongeza ya asilimia 25 kwenye zawadi za fedha kwa washindi wa mbio za kilometa 42 za Kilimanjaro Premium Lager Marathon, ambapo jumla ya zawadi ya fedha itaongezeka kutoka Tsh milioni 15 hadi Tsh milioni 20, huku washindi wa kwanza, wa pili na wa tatu wanaume kwa wanawake wakipokea jumla ya Tsh milioni nane na kiasi kilichobaki kikigawanywa miongoni mwa washindi wanne hadi wa 10.
    Kavishe alisema kwamba ni bahati kubwa kwa Kilimanjaro Premium Lager kudhamini mashindano haya yenye msisimko mkubwa katika kalenda ya michezo nchini Tanzania na kwamba Bia ya Kilimanjaro Premium Lager itatoa zawadi kubwa za fedha kwa wanariadha wakati wengine watabaki wana kumbukumbu isiyofutika ya ukaribu wa hali yajuu.
    Ili kuwahamasisha na kuwapa motisha wanariadha wa Tanzania kuongeza viwango vyao na kutumia muda mfupi kumaliza mbio hizo, Kilimanjaro Premium Lager imetenga Shilingi milioni mbili kama bonasi au malipo ya nyongeza kwa wanariadha wa Tanzania watakaovunja rekodi kwenye mashindano hayo.
    Zawadi zitakazotolewa kwenye 2014 Kilimanjaro Marathon zimenyumbulishwa kitakwimu kama ifuatavyo hapa chini;

    2014 KILI MARATHON PRIZES
    2013 KILI MARATHON PRIZES

    MALE
    FEMALE

    MALE
    FEMALE
    1ST
    4,000,000
    4,000,000
    1ST
    3,000,000
    3,000,000
    2ND
    2,000,000
    2,000,000
    2ND
    1,500,000
    1,500,000
    3RD
    1,000,000
    1,000,000
    3RD
    850,000
    850,000
    4TH
    900,000
    900,000
    4TH
    650,000
    650,000
    5TH
    600,000
    600,000
    5TH
    500,000
    500,000
    6TH
    400,000
    400,000
    6TH
    350,000
    350,000
    7TH
    350,000
    350,000
    7TH
    250,000
    250,000
    8TH
    300,000
    300,000
    8TH
    200,000
    200,000
    9TH
    250,000
    250,000
    9TH
    150,000
    150,000
    10TH
    200,000
    200,000
    10TH
    100,000
    100,000






    SUB TOTAL
    10,000,000
    10,000,000
    SUB TOTAL
    7,550,000
    7,550,000






    GRAND TOTAL

    20,000,000
    GRAND TOTAL

    15,100,000

    Bendera juu; Ole Gabriel na Nyambui kulia 

    Mkurugenzi wa Masoko Vodacom, Kevin Twisa akihutubia katika hafla hiyo

    Meneja wa Bia ya Kilimanjaro, George Kavishe akihutubia

    Mjadala; Kutoka kulia Kevin Twisa, Mama Juliana Yassoda kutoka Wizara ya Habari na Salum Mwalimu 

    Nyambui akihutubia

    Ole Gabriel akihutubia

    Kikundi cha sanaa cha THT kikiwasilisha bendera kwa mbwembwe za kisanii

    Mazungumzo; Kutoka kulia Mkurugenzi Mkuu wa Executive Solutions, Aggrey Marealle akijadiliana jambo na Meneja wa Kilimanjaro Beer, George Kavishe na Meneja Matukio wa kampuni yake (Executive), Glory Chuwa 

    Nyambui akifurahia jambo na Ofisa wa Executive, Michael Mukunza kulia

    Mama Yassoda akimkabidhi cheti, Ibrahim Kyaruzi wa Executive Solutions kutambua mchango wa kampuni hiyo katika historia ya mbio hizo za kimataifa 
    Kavishe alisema anatarajia kwamba zawadi hizo za fedha zitawavutia wanariadha mashuhuri na kuwapa moyo wengine kuvunja rekodi za mashindano hayo.
    Aliongeza kwamba Kilimanjaro Marathon imepiga hatua kutoka tukio la mkoa hadi kuwa mashindano makubwa ya kimataifa. “Tunatambuliwa na IAAF na Chama cha Kimataifa cha Mbio za masafa Marefu. Licha ya mafanikio haya, tunaendelea kujitahidi kuboresha mbio hizi mwaka hadi mwaka,” alisemaKavishe.
    Tunashukuru kwa jinsi walivyoungwa mkono na Wizara ya Michezo na mamlaka za Serikali ya Mkoa wa Kilimanjaro, Riadha Tanzania, Chama cha Mbio za Ridhaa Kilimanjaro, pamoja na wadhamini wenzawao ambao ni GAPCO, Simba Cement, CFAO Motors, KK Security, Keys Hotel, TPC Sugar, FNB Bank na Kilimanjaro Water kwa kusaidia kuikuza Kilimanjaro Marathon kuwa moja ya mashindano makubwa zaidi ya mbio za masafa marefu barani Afrika.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: KILI MARATHON 2014 YAZINDULIWA LEO, ZAWADI SI MCHEZO Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top