KOCHA Jose Mourinho amesema kwamba John Terry anaweza kuwa amestaafu mapema mno kuchezea timu ya taifa ya England, huku akithibitisha Gary Cahill, mbadala wake katika kikosi hicho ataendelea kusubiri Chelsea kwa mkongwe huyo.
Terry alistaafu timu ya taifa miezi 13 iliyopita, siku chache kabla ya FA kumkuta na hatia ya kumfanyia vitendo vya kibaguzi Anton Ferdinand.
Cahill amejihakikishia namba katika kikosi cha kwanza Roy Hodgson, lakini Mourinho anampa nafasi Terry kucheza pamoja na David Luiz katika ukuta wa Chelsea. Inamaanisha Cahill anaiweka rehani nafasi yake ya kuwamo katika kikosi cha England kitakachokwenda Brazil kwenye Fainali za Kombe la Dunia kwa kusugua benchi kuanzia leo mechi na Cardiff.
"Kama ningekuwa mchezaji wa mpira, ningesubiri timu ya taifa wasema: "Hatukuhitaji tena", alisema Mourinho. "Lakini hizo ni hisia zanu binafsi. NingesubiriI, kwa ukweli. Lakini alikuwa ana sababu za kumsukuma kuchukua uamuzi huo,".
Anajenga timu: Jose Mourinho anaongoza moja ya vikosi vya nguvu Ulaya
Chaguo la kwanza: John Terry na David Luiz ndio chaguo la kwanza la Mourinho
Nahodha wa zamani England: Terry alirithi beji ya Unahodha England kutoka kwa David Beckham
0 comments:
Post a Comment