WINGA wa AC Milan na Italia, Stephan El Shaarawy alipigwa picha akiwa na kibegi anakatiza jiji la Manchester katika kitongoji cha Chorlton Alhamisi usiku.
Mshambuliaji huyo kinda amekuwa kihusishwa kwa kiasi kikubwa na kuhamia Manchester City na kuonekana kwake katika saluni mjini humo kunazalisha swali, alikufanya anafanya nini?
Bahati mbaya kwa mashabiki wa City, jibu halihusiani kabisa na uhamisho wake - kwani alikuwa huko kwa ajili ya kupiga picha za video ya tangazo jipya la biashara la Samsung kwa ajili ya Televisheni.
Tangu aibuke katika kikosi cha kwanza mwaka 2011 akiwa na umri wa miaka 18 tu, El Shaarawy amekuwa mmoja wa wachezaji teemeo wa AC Milan.
Mshambuliaji wa zamani wa Man City, Mario Balotelli aliungana na mchezaji huyo mwaka jana katika klabu hiyo na kwa pamoja wawili hao wamepewa jina 'sura za Italia mpya', wakiwa kivutio katika ligi kwa mfumo wao wa maisha na aina ya uchezaji wao.
Kutoka Milan hadi Chorlton: El Shaarawy ni mchezaji wa kikosi cha kwanza Milan - na inaonekana atabaki huko
Waili wa utani: Mshambuliaji wa zamani wa Man City, Mario Balotelli na El Shaarawy ni marafiki wazuri, na wanacheza pamoja katika klabu na timu ya taifa
0 comments:
Post a Comment