Mtibwa Sugar |
Na Princess Asia
LIGI Kuu ya Vodacom Tanzania
Bara inatarajiwa kuendelea leo kwa mchezo mmoja tu utakaopigwa kwenye Uwanja
Chamazi, Dar es Salaam, kati nya Ruvu Shooting ya Pwani na Mtibwa Sugar ya
Morogoro.
Mechi hiyo ilitakiwa
kuchezwa kwenye Uwanja wa Mabatini, Mlandizi lakini kwa sababu ya kuonyeshwa
moja kwa moja na Televisheni ya Super Sport ya Afrika Kusini umehamishiwa
Uwanja wa Azam.
Unatarajiwa kuwa mchezo
mzuri usio na jakamoyo na bila shaka watakaoushuhudia kupitia Super Sport
watafurahia soka ya kuvutia. Mechi nyingine za ligi hiyo zilichezwa mwishoni
mwa wiki, kuanzia Ijumaa na kurushwa pia moja kwa moja na Super Sport.
Katika mchezo wa jana, Yanga ilishinda mabao 3-1
dhidi ya African Lyon Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, shukrani kwake kiungo
anayecheza kwa nadra kwenye timu hiyo, Nizar Khalfan aliyefunga mabao ya
ushindi dakika ya 65 na 88, akitokea benchi kuchukua nafasi ya Frank Domayo.
Nizar alifunga bao la pili, sekunde chache baada ya Benedictor
Mwamlangala kuisawazishia African Lyon bao lililodumu tangu dakika ya 17, baada
ya Nahodha wa Yanga, Nadir Haroub ‘Cannavaro’ kutangulia kufunga dakika ya 17.
Ushindi huo, unaifanya Yanga ifikishe pointi saba,
baada ya kucheza mechi nne na kupanda hadi nafasi ya nne kwenye msimamo wa
ligi, ikiwa inalingana na Coastal kwa pointi na wastani wa mabao, ingawa
Coastal wako nyuma kwa mechi moja.
Simba iliichapa Prisons ya Mbeya iliyorejea Ligi Kuu
msimu huu mabao 2-1, yaliyotiwa kimiani na Felix Mumba Sunzu na Mrisho Ngassa,
wakati la Prisons lilifungwa na Elias Maguri.
Simba bado inaongoza ligi hiyo, kwa pointi zake 12,
ikifuatiwa na Azam iliyoifunga JKT Ruvu 3-0 Ijumaa, mabao ya John Bocco ‘Adebayor’,
Kipre Herma Tchetche na Kipre Michael Balou yenye pointi 10.
0 comments:
Post a Comment