// Disable text selection (not fully reliable) function disableSelection(element) { element.setAttribute('unselectable', 'on'); element.style.userSelect = 'none'; element.style.MozUserSelect = 'none'; element.style.webkitUserSelect = 'none'; } // Apply to the entire document body document.addEventListener('DOMContentLoaded', function() { disableSelection(document.body); }); BENZEMA APIGA MBILI, ASETI MBILI UFARANSA IKIIFUMUA JAMAICA 8-0 - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE BENZEMA APIGA MBILI, ASETI MBILI UFARANSA IKIIFUMUA JAMAICA 8-0 - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE
  • HABARI MPYA

    Monday, June 09, 2014

    BENZEMA APIGA MBILI, ASETI MBILI UFARANSA IKIIFUMUA JAMAICA 8-0

    UFARANSA wanakwenda Brazil kiroho safi baada ya jana kuichapa Jamaica mabao 8-0 katika mchezo wa mwisho wa kujipima kabla ya kuanza kwa michuano hiyo wiki hii.
    Mshambuliaji wa Real Madrid, Karim Benzema alifunga mabao mawili, akapika mawili pia, la nne lililofungwa na Oliver Giroud na la pili lililofungwa na kiungo Blaise Matuidi. Mutuidi naye alimsetia Benzema bao lake la pili. 
    Winga nyota, Franck Ribery ameondolewa kwenye kikosi cha Ufaransa kwa sababu ya majeruhi, lakini bado Les Blues imeendelea kung'ara. 

    Mtu mzima yuko vizuri: Benzama akishangilia bao lake la kwanza na la tatu kwa Ufaransa jana ikiichapa Jamaica 8-0 mjini Lille
    Deadly: Benzema scored both his goals from the corner of the box cutting in from the left hand side
    Shuti: Benzema alifunga mabao tote akiwa pembeni kwa boksi mkono wa kushoto

    Giroud alimsetia bao la kwanza kiungo Yohan Cabaye, beki wa kushoto, Patrice Evra alimmiminia krosi Matuidi kufunga la pili usiku huo, na Antoine Griezmann alitokea benchi kufunga mabao mawili matamu. 
    Kiasi cha mwaka mmoja uliopita, Benzema alikuwa anasotea nafasi kikosi cha kwanza baada ya kucheza mechi 15 bila kufunga, lakini sasa amefunga mabao sita katika mechi sita zilizopita alizoichezea Ufaransa hivyo kufikisha junla ya mabao 21 katijka mechi zote 66 akiwa na jezi ya Les Blues. 
    Huu ulikuwa ushindi mkubwa wa kwanza wa Ufaransa tangu waifunge 10-0 Azerbaijan mwaka 1995. 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: BENZEMA APIGA MBILI, ASETI MBILI UFARANSA IKIIFUMUA JAMAICA 8-0 Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top