• HABARI MPYA

    Thursday, April 19, 2012

    PATNA WA AY MAMTONI AACHIA KITU KIPYA KIKALI

    La Myia
    MSANII La'Myia, mzaliwa wa Panorama City, California mtoto wa Tyra Doyle na Leon Good, ameiambia bongostaz.blogspot.com kwamba ametoa wimbo mpya.
    Amejitambulisha kama dada wa mwigizaji Meagan Good na mpwa wa mwimbaji na mwigizaji Dijon Talton.
    Mwaka 2001, alitoa wimbo Good akiwa na LeTecia Harrison, Ardena Clark na Quierra Davis-Martin ambao walianzisha kundi la R&B lililoitwa Isyss.
    Wakiwa kama kundi mwaka 2002 walitoa albamu "The Way We Do", ambayo ilijumuisha nyimbo zilizoingia kwenye chati za Hot 100 kama "Day & Night" waliomshirikisha rapa Jadakiss na "Single For The Rest Of My Life". Wamewahi kuingizwa kwenye kinyang’anyiro cha tuzo mbili za Soul Train Lady of Soul na walishinda tuzo moja.
    Bahati mbaya walipigwa chini na lebo ya Arista Records kutokana na mauzo mabaya ya albamu yao kabla hawajatoa albamu yao ya pili.
    Albamu yao pekee "The Way We Do" ilishika namba 55 katika chati za Billboard na kuuza nakala 300,000.
    Baada ya kuachana na kundi hilo mwaka 2006, Good na "Love" wote walijiunga na kundi jipya la R&B, lililojulikana kama BAD GYRL.
    Mwaka 2011 aliimba wimbo Speak Wit Ur Body wa AY wa  Tanzania, ambao alimshirikisha pia Good na Romeo Miller.
    Mwaka 2012 alitoa wimbo wake mpya ulioitwa Graduate Me akimshirikisha Tyga (Young Money Cash Money Brother).
    Good pia ni mwigizaji na ameshiriki show mbalimbalin za TV kama Tall Hopes, Sister, Sister, The Parent 'Hood, Smart Guy, ER, The Parkers na Judging Amy.
    Pia amecheza filamu kama The Wood na  Busted iliyotoka karibuni.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: PATNA WA AY MAMTONI AACHIA KITU KIPYA KIKALI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top