• HABARI MPYA

    Wednesday, April 18, 2012

    DROOOGBAAAAAAAAAAAAAAA, BARCA CHALI DARAJANI

    Mfalme Didier Yves Droba
    Sterling wa picha la leo Didier Yves 'Tito' Drogba
    Ukisikia kamata mwiiizi meen, ndio hii Lampard na Messi
    Messi chini ya ulinzi wa kutosha
    Drogba alikuwa ''Messi" leo

    Frank Lampard (kushoto) akimdhibiti Andres Iniesta.
    Obi ng'ado kwa ng'ado na mtu
    Msitu wa Barca ukidhibitiwa na mwanaume mmoja tu wa Chelsea
    Mshambuliaji wa Chelsea, Didier Drogba akishangilia bao lake pekee alilofunga dakika ya pili ya dakika za majeruhi baada ya kutimu dakika 45 za kipindi cha kwanza kwenye Uwanja wa Stamford Bridge, London, England usiku huu katika Nusu Fainali ya Kwanza ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, dhidi ya mabingwa watetezi, Barcelona ya Hispania. Chelsea sasa inahitaji sare yoyote kwenye mchezo wa marudiano ugenini, Uwanja wa Camop Nou ili kutinga fainali, ambako itacheza na mshindi kati ya Bayern Munich ya Ujerumani na Real Madrid ya Hispania. Mechi ya kwanza jana mjini Munich, Real walifungwa 2-1 na wanahitaji ushindi japo wa 1-0 nyumbani, Santiago Bernabeu ili kutinga Fainali.


    MUHIMU KUJUA HAYA...
    •The Blues wameendeleza rekodi nzuri ya nyumbani msimu huu katika Ligi ya Mabingwa, leo wakishinda mechi ya saba katika mechi saba walizocheza, wamefunga mabao 17 na wamefungwa mawili tu.

    •Leo ni mara ya saba kwa timu hiyo ya London kucheza Nusu Fainali ya Ligi ya Mabingwa ndani ya miaka tisa.

    Lakini wameshinda mechi moja tu, walipoifunga kwa jumla ya mabao 4-3 mwaka 2008. Je, wataitoa Barca Camp Nou?

    •Timu hiyo ya Stamford Bridge haijawahi kutwaa Kombe lolote la Ulaya, zaidi ya kushika nafasi ya pili mwaka 2008.

    •Barcelona ilipokwenda mara ya mwisho London, Mei mwaka jana kwenye Uwanja wa Wembley, iliifunga Manchester United mabao 3-1 na kutwaa taji la nne la Ligi ya  Mabingwa.

    •Kama mabingwa hao watetezi watatwaa taji hilo msimu huu, itakuwa mara ya nne ndani ya miaka saba na itakuwa timu ya kwanza kutetea taji tangu AC Milan mwaka 1990.

    •Kabla ya leo, timu ya mwisho kuifunga Barca katika michuano hii, ilikuwa ni Inter Milan chini ya Jose Mourinho ambaye sasa anaikochi Real Madird mwaka 2010.

     •Leo Lionel Messi ametimiza mechi saba anakutana na Chelsea katika Ligi ya  Mabingwa bila kutikisa nyavu za The Blues.

    •Wakati timu hizo zilipokutana katika Robo Fainali mwaka 2000, Barcelona iliifunga Chelsea 5-1 katika mechi ya marudiano Uwanja wa Camp Nou.

    Katika mechi hiyo, Roberto Di Matteo alicheza kwenye kikosi cha kwanza cha The Blues, wakati Pep Guardiola alichezea Barca- leo wote wanakaa kwenye mabenchi ya timu zao.

    •Kabla ya leo, Chelsea ilikutana mara ya mwisho na Barcelona Mei mwaka 2009, kwenye michuano kama hii na hatua kama hii. Baada ya sare ya bila kufungana kwenye  mechi ya kwanza, Barca walifuzu kuingia fainali kwa bao la dakika ya mwisho la Andres Iniesta, ambalo lilikuwa la kusawazisha baada ya Michael Essien kutangulia kufunga. Barca ilifuzu kwa faida ya bao la ugenini.

    VIKOSI VILIVYOCHEZA LEO:
    Chelsea: Cech, Ivanovic, Cahill, Terry, Cole, Mikel, Lampard, Meireles, Ramires/Bosingwa dk88, Mata/ Kalou dk 74 na Drogba.
    Wa akiba ambao hawakutumika:
    Turnbull, Essien, Torres, Malouda, Sturridge
    WALIOPEWA KADI ZA NJANO:
    Cheldes: Ramires, Drogba
    MFUNGAJI WA BAO: Drogba dakika ya 45
    Barcelona: Valdes, Dani Alves, Puyol, Mascherano, Adriano, Busquets, Iniesta, Xavi/Cuenca dk86, Messi, Sanchez/Pedro dk66 na Fabregas/Thiago dk78. Subs WA AKIBA AMBAO HAWAKUTUMIKA:
    Pinto, Pique, Bartra, Keita
    WALIOPEWA KADI ZA NJANO:
    Pedro, Busquets.
    MAHUDHURI: 38,039
    REFA: Felix Brych (Ujerumani).
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: DROOOGBAAAAAAAAAAAAAAA, BARCA CHALI DARAJANI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top