• HABARI MPYA

    Friday, April 13, 2012

    ALIYEMLETA MANJI YANGA KUAGWA JUMATATU KIJICHI

    Marehemu Rutta
    MWILI wa mjumbe wa kamati ya Utendaji ya klabu ya Yanga Theonest Rutashoborwa (pichani)unatarajiwa kuagwa jumatatu ijayo katika kanisa katoliki parokia ya kijichi kabla ya kusafirishwa kwenda kwao kijiji cha Bukabaye kilicopo Bukoba mkoani Kagera.
    Kwa mujibu wa mamapipiro.blogspot, Rutashoborwa ambaye kitaaluma ni wakili akimiliki kampuni ya Brilliance Law Chambers ya jijini Dar es Salaam alikutwa na umauti huo usiku wa kuamkia leo katika hospitali ya Agha Khan alipokwenda baaada ya kujisikia vibaya kabla ya kubainika kuwa na kisukari na shinikizo la damu.
    Ofisa habari wa Yanga, Louis Sendeu amesema kuwa Rutashoborwa alianza kujisikia vibaya mara alipotua uwanja wa ndege wa mwalimu Jk Nyerere akitokea Moshi, Kilimanjaro alipokwenda kwa shughuli zake za kikazi na alipokimbizwa hoispitalini alifariki akiwa katika harakati za kupelekwa chumba cha uangalizi maalum (ICU).
    “Yanga inasikitisha kumpoteza kiongozi huyu hidari ambaye alikuwa muhimili mkuu katika kuinganisha Yanga, kwa nianba ya wanachama na wapenzi wa Yanga tunatoa pole kwa familia ya marehemu, ndugu jamaa na marafiki,”Alisema Sendeu.
    “Marehemu ameacha mjane na watoto wanne, bwana ametoa Bwana ametwaa, mwenyezi mungu aiweke rioho ya marehemu mahali pema peponi, Amin,”Alisema.
    Rutashoborwa atakumbukwa sana Yanga, kutokana na jitihada zake zilizosaidia klabu hiyo kumpata mfadhili, Yussuf Manji mwaka 2006.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: ALIYEMLETA MANJI YANGA KUAGWA JUMATATU KIJICHI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top