• HABARI MPYA

    Friday, April 13, 2012

    DI MATTEO AWAPA 'MAKAVU LIVE' MABOSI FA ENGLAND

    Di Matteo
    KAIMU kocha wa Chelsea, Roberto Di Matteo amesema leo kwamba yanahitajika mabadiliko katika hatua za kinidhamu zinazochukuliwa na Chama cha Soka England (FA), baada ya klabu yake kupata pigo kwa mchezaji wake, Branislav Ivanovic kuadhibiwa.
    Di Matteo anaamini FA ilikosea kumtia hatiani Ivanovic kwa kumchezea rafu kiungo wa Wigan, Shaun Maloney, wakati mshambuliaji wa Manchester City, Mario Balotelli hakuadhibiwa kwa kumchezea rafu Alex Song wa Arsenal.
    Ivanovic amefungiwa mechi tatu, na ataikosa Nusu Fainali ya Kombe la FA Jumapili dhidi ya Tottenham, baada ya FA kutumia udhahidi wa video kumtia hatiani beki huyo wa Serbia.
    Di Matteo anashawishika kwamba taratibu za FA hazina uhakika wanapochukua uamuzi ambao unaziathiri klabu.
    "Nafkiri kila mtu anatazamia maamuzi ya uhakika kutoka FA. Hicho ndio muhimu kwa kila mtu, wadau wote wakiwemo - uhakika," alisema.
    "Wangerudia maamuzi wanayotoa na adhabu wanazotoa, na ni matumaini kwamba wangekuja na maamuzi ya usawa zaidi."alisema.
    Di Matteo pia alitaka ushahidi wa video utumike kwa mapama marefu zaidi, akitolea mfano wa tukio la Ivanovic: "Unaangalia katika picha na unafikiri: 'Tunatumia picha za video kwa hilo, sawa, lakini kwa nini hatukutumia teknolojia ya kwenye goli'.
    "Kwa nini hapana? Kama tumetumia hii kwa ajili ya hilo, kwa nini tusitumie hiyo kwa mabao? Hivyo, ni kwa nini inapaswa kutazamwa upya (taratibu za adhabu za FA). Inatakiwa kuwa ya haki zaidi na usawa.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: DI MATTEO AWAPA 'MAKAVU LIVE' MABOSI FA ENGLAND Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top