• HABARI MPYA

    Friday, April 13, 2012

    KANUMBA AMLIZA ASIA, AANGUA KILIO KUTOKA MAREKANI

    Asia kulia, Sharifa kushoto walipokuwa na Kanumba katikati Marekani Januari mwaka jana
    MBUNIFU wa mavazi nchini Asia Idarous ambaye kwa sasa yuko Marekani, amedai kushtushwa sana na msiba wa msanii Steven Kanumba.
    Akizungumza na bongostaz kutoka Marekani, Asia alisema ameshitushwa sana na msiba huo.
    Pamoja na kushitushwa huko, pia ameelezwa kuhuzunishwa na kukosa nafasi ya kuja nchini kuhudhuria mazishi yake.
    Akielezea jinsi alivyopokea taarifa hizo, Asia alisema alikuwa katika moja ya maonyesho yake Mjini Dallas na hivi karibuni na wakati anatoka nje ya ukumbi akadokezwa kuwa Kanumba amefariki.
    “Nilikuwa kwenye onyesho langu la Lady In Redy nchini Marekani na wakati natoka nje nikapewa taarifa hizo za msiba, kiukweli imeniumiza sana kwa kuwa Kanumba alikuwa kama mwanangu,” alisema Asia.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: KANUMBA AMLIZA ASIA, AANGUA KILIO KUTOKA MAREKANI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top