• HABARI MPYA

    Friday, November 04, 2016

    SIMBA WAIPUNGUZIA BEI YANGA ISHU YA KESSY...SASA YATAKA MILIONI 200 TU!

    Na Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM
    SIMBA SC imepunguza bei ya mchezaji Hassan Ramadhan Kessy kutoka Sh. Bilioni 1.2 hadi Sh. Milioni 200 baada ya kikoa cha juzi ofisi za Shirikisho la Soka Tanzania (TFF).
    Ofisa Habari wa TFF, Alfred Lucas amesema leo katika mkutano na Waandishi wa Habari kwamba, japokuwa msuluhishi mteule, Mwenyekiti wa zamani wa TFF enzi za FAT (Chama cha Soka Tanzania), Said El Maamry hakuhudhuria, lakini kikao kilikwenda vizuri.
    Lucas alisema kwamba Yanga iliwakilishwa na Kaimu Katibu Mkuu wake, Baraka Deusdedit, Mjumbe wa Kamati ya Utendaji, Omar Said na Mawakili Oscar Magolosa na Alex Mushumbusi, wakati Simba iliwakilishwa na Mwenyekiti wake wa Kamati ya Usajili, Zacharia Hans Poppe.
    “Kwa hali halisi ya uchumi kwa sasa, timu hizo zimezungumza hadi kufikia mwafaka wa kiwango kisichozidi Sh milioni 200 kutoka dola 600,000 (zaidi ya Sh. Bilioni 1.2),”alisema Lucas na kuongeza; “Mazungumzo ya wikiendi hii yanakwenda kukamilisha mvutano wao, kama ambavyo walikubaliana kwenye kikao cha jana (juzi),”.
    Katika kesi hiyo, Simba inamlalamikia Kessy kujiunga na Yanga kabla ya kumaliza Mkataba wake, hivyo mchezaji amevunja Mkataba na anatakiwa kulipa Sh. Bilioni 1.2 ambazo sasa zimeshushwa hadi Milioni 200.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: SIMBA WAIPUNGUZIA BEI YANGA ISHU YA KESSY...SASA YATAKA MILIONI 200 TU! Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top