• HABARI MPYA

    Wednesday, November 28, 2012

    MACHO YOTE KWA JOHN BOCCO ADEBAYOR WA CHAMAZI LEO

    John Bocco 'Adebayor'

    Na Mahmoud Zubeiry, Kampala
    MSHAMBULIAJI tegemeo wa Tanzania, John Bocco ‘Adebayor’ bado anaongoza kwa mabao katika michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki, CECAFA Tusker Challenge baada ya mechi 14 kuchezwa hadi hadi jana.
    Jumla ya mabao 15 hadi sasa yamefungwa katika mechi 14 za makundi yote matatu, zilizopigwa kwenye Uwanja wa Mandela, Namboole, Kampala.
    Bocco anachuana kwa ufungaji na washambuliaji wa Burundi, Chris Nduwarugira na Suleiman Ndikumana, ambao kila mmoja ana mabao mawili pia.
    Wengine ambao hadi sasa kila mmoja amefunga bao moja ni Yussuf Ndikumana wa Burundi, Mohamed Jabril wa Somalia kwa penalti, Geoffrey Kizito wa Uganda, Yonatal Kebede Teklemariam, Haruna NiyonzimUganda, David Ochieng, Clifton Miheso na Jean Mugiraneza.
    Bocco ana nafasi zaidi ya kuongeza mabao katika mechi za kundi hilo, haswa kwenye mchezo dhidi ya Somalia Desemba 1, kwani hiyo ndio timu dhaifu zaidi kwenye Kundi B.
    Lakini Bocco kama atacheza kwa kiwango cha mechi dhidi ya Sudan, anaweza akawa mwiba hata leo mbele ya Burundi.
    Kwa sasa Bocco anayechezea Azam FC ya Dar es Salaam, ndiye mshambuliaji pekee kwenye kikosi cha Bara, baada ya washambuliaji wengine, Mbwana Samatta na Thomas Ulimwengu wanaochezea TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemomkrasia ya Kongo (DRC) kuzuiliwa na klabu yao.

    WAFUNGAJI CECAFA TUSKER CHALLENGE 2012
    John Bocco                   Tanzania  2
    Yussuf Ndikumana        Burundi    2
    Suleiman Ndikumana    Burundi    2
    Yussuf Ndikumana        Burundi   1
    Mohamed Jabril             Somalia   1(penalti).
    Geoffrey Kizito               Uganda   1
    Brian Umony                  Uganda   1
    Yonatal Teklemariam     Ethiopia   1
    Haruna Niyonzima         Rwanda   1
    Jean Mugiraneza           Rwanda   1
    David Ochieng               Kenya      1
    Clifton Miheso                Kenya      1
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: MACHO YOTE KWA JOHN BOCCO ADEBAYOR WA CHAMAZI LEO Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top