• HABARI MPYA

    Monday, November 26, 2012

    YANGA KWENDA UTURIKI KUPIGA KAMBI YA WIKI MBILI, BRANDS APANDISHA MAKINDA MATATU YA B YANGA A

    Mwenyekiti wa Kamati ya Mashindano ya Yanga, Abdallah Ahmad Bin Kleb (kushoto) akizungumza na Waandishi wa Habari, makao makuu ya klabu, makutano ya mitaa ya Twiga na Jangwani, Dar es Salaam leo. Kulia ni Kocha Mkuu wa klabu hiyo, Mholanzi, Ernie Brandts. Picha na Princess Asia

    Na Princess Asia
    KATIKA kujiandaa na mzunguko wa pili wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, Yanga ya Dar es Salaam inatarajia kwenda kuweka kambi ya wiki mbili nchini Uturuki mapema mwakani.
    Mwenyekiti wa Kamati ya Mashindano ya Yanga, Abdallah Ahmad Bin Kleb amesema leo katika Mkutano na Waandishi wa Habari, makao makuu ya klabu, makutano ya mitaa ya Twiga na Jangwani, Dar es Salaam kwamba ziara hiyo inatarajiwa kufanyika kati ya Desemba na  Februari 25, mwakani.
    Alisema pendekezo la kambi hiyo lilitolewa na kocha mkuu wa Yanga, Mholanzi Ernie Brandts ambaye ana uzoefu na nchi hiyo ambayo ina vitu vinavyostahili kwa ajili ya timu kuweka kambi.
    Alisema ikiwa huko timu hiyo inatarajiwa kucheza mechi mbili za kitrafiki na timu zitkazotajwa baadaye.
    Aidha, kocha mkuu wa timu hiyo amewapandisha wachezaji watatu wa kikosi cha vijana chini ya miaka 20 wakiwemo kipa, Yussuf Abdallah, George Banda na Rehan Kibinga.
    Katika hatua nyingine, Bin Kleb aliasema wanajivunia uongozi wa sasa chini ya Mwenyekiti, Alhaj Yussuf Manji, kwani timu imekuwa na mafanikio makubwa ikiwemo kutwaa kombe la Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, Kagame, kufanya vema katika mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu ambao ulimalizika kwa timu kuongoza.
    Alisema kufanya vizuri katika Ligi Kuu, ni matunda ya timu hiyo kuweka kambi nchini Rwanda baada ya Kombe la Kagame.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: YANGA KWENDA UTURIKI KUPIGA KAMBI YA WIKI MBILI, BRANDS APANDISHA MAKINDA MATATU YA B YANGA A Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top