• HABARI MPYA

    Tuesday, November 27, 2012

    ANELKA KUTUA QPR JANUARI AKIJUTIA KWENDA CHINA


    KOCHA mpya wa Queens Park Rangers, Harry Redknapp anataka kumsajili Nicolas Anelka Januari mwakani.
    Redknapp atapewa pauni Milioni 10 za kusajili katika dirisha dogo, lakini atahitaji fedha zaidi ili kuingia sokoni.
    Loan ranger: QPR want Nicolas Anelka to boost their survival bid
    Nicolas Anelka 
    Kocha huyo mwenye umri wa miaka 65 anafahamu anatakiwa kuboresha safu yake ya ushambuliaji kutokana na kukabiliwa na majeruhi Andrew Johnson na Bobby Zamora, wanaomfanya abaki na Djibril Cisse kama mshambuliaji pekee.
    Na Redknapp amemtambulisha mshambuliaji huyo wa zamani wa Chelsea, Anelka kama mtu anayemtaka kwa mkopo.
    Mkongwe huyo mwenye umri wa miaka 33 ana mkataba na  Shanghai Shenua, lakini anaweza kurejea kuwa muda kucheza England, baada ya kumalizika kwa Ligi Kuu ya China.
    Anelka kwa ujumla yuko tayari kurejea Ulaya baada ya kusema alifanya kosa kuhamia China.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: ANELKA KUTUA QPR JANUARI AKIJUTIA KWENDA CHINA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top