• HABARI MPYA

    Thursday, April 05, 2012

    SETIF WATAKA KUGOMEA MECHI KWAO

    ES Setif
    WACHEZAJI wa timu ya soka ya ES Setif wametishia kugomea mechi yao dhidi ya Simba endapo hawatalipwa mishahara yao ya mwezi uliopita.
    Wachezaji hao wametangaza mgomo huo ikiwa zimebaki saa chache tu, kabla hawajacheza na Simba mechi ya pili ya hatua ya awali ya michuano ya Kombe la Shirikisho inayotarajiwa kuchezwa kesho.
    Gazeti la Habari Leo, limeandika kwamba Habari kutoka Algeria zinasema, nahodha wa timu hiyo Mourad Delhoum aliyezungumza kwa niaba ya wenzake alisema taarifa hizo wameziwasilisha kwa uongozi wa klabu hiyo.
    Madai makubwa ya wachezaji hao mishahara yao pamoja na posho za ligi ya ndani na michuano ya kimataifa ambapo walikumbusha kuwa waliwaonya viongozi wao walipokuwa
    Dar es Salaam kucheza na Simba wiki mbili zilizopita kwamba wanataka walipwe fedha zao.
    Na kwamba waliahidiwa wangelipwa fedha zao baada tu ya kuwasili Algeria lakini mpaka juzi suala hilo halikuwepo.
    Kiongozi wa timu hiyo, Hakim Serrar alikuwa safarini Algiers kuhudhuria kikao cha viongozi wa klabu, lakini alilazimika kuahirisha safari hiyo baada ya kuona kwenye vyombo vya habari kwamba wachezaji wameanza mgomo.
    Kutokana na hilo, shughuli zote za klabu hiyo zilisimama tangu juzi mpaka hapo uamuzi mwingine utakapotolewa na uongozi ulikuwa ukifanya jitihada kuwalipa wachezaji chao.
    Hata hivyo, viongozi wana muda mfupi sana kutafuta fedha kwa ajili ya kulipa wachezaji wao kabla ya kukutana na Simba kesho na kama hazitapatikana na wachezaji wakaendelea na mgomo wao kuna hatari ya kufungiwa kushiriki michuano ya kimataifa kwa miaka miwili.
     Hakim Serrar hakufanya siri kulizungumzia hilo kama tatizo kubwa katika historia ya SSE, na pia hakuficha kwamba wachezaji walikuwa na haki ya kufanya uamuzi waliofikia.
    Simba iliondoka jijini Jumapili kuelekea Setif itakapochezwa mechi hiyo kesho ambapo kabla ya kuelekea Algeria kwanza walilala Cairo, Misri na Jumanne kuelekea Setif.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: SETIF WATAKA KUGOMEA MECHI KWAO Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top