• HABARI MPYA

    Saturday, November 05, 2016

    MCHEZO KATI YA BULYANHULU, GREEN WARRIORS

    Na Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM
    MCHEZO namba 4 wa Ligi Daraja la Pili kati ya Bulyanhulu na Green Warriors ulikuwa ufanyika jana Novemba 4, 2016 kwenye Uwanja wa CCM-Kambarage, mkoani Shinyanga haikufanyika.
    Mchezo huo haikufanyika kwa sababu ya kukosa mawasiliano kati ya msimamzi wa kituo huko Shinyanga, Kamisaa na Mchezo na Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF).
    Kwa taarifa hii, TFF inapenda kufahamisha familia ya mpira wa miguu kuwa mchezo huo utafanyika hapo baadaye kwa kupangiwa tarehe nyingine mpya baada ya kuondolewa kwa changamoto inayohusu leseni za wachezaji ambazo ziko tayari shirikishoni.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MCHEZO KATI YA BULYANHULU, GREEN WARRIORS Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top