Na Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM
KOCHA mpya wa Toto Africans ya Mwanza, Khalfan Ngassa ‘Babu’ ameanza vyema baada ya kuiwezesha timu hiyo kuibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya wenyeji Kagera Sugar Uwanja wa Kaitaba, Bukoba katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara leo.
Pongezi kwao wafungaji wa mabao hayo, Jamal Soud dakika ya 47 na Mohamed Soud dakika ya 80, waliomtungua kipa wa zamani wa Simba SC ya Dar es Salaam, Hussein Sharrif ‘Casillas’.
Khalfan Ngassa ‘Babu’ (kushoto) akiwa na mchezaji mwenzake wa zamani wa Pamba na Simba, Juma Amir Maftah
Huo ulikuwa mchezo wa kwanza Toto ikicheza chini ya kocha mpya, Khalfan Ngassa baada ya kuondolewa kwa Rogasian Kaijage aliyekuwa kocha wa timu tangu mwanzo wa msimi baada ya kuondolewa kwa John Tegete.
Kwa matokeo hayo, Toto inafikisha point inane baada ya kucheza mechi nane, huu ukiwa mchezo wa pili kushinda baada ya kufungwa mechi nne na kutoa sare mbili.
KOCHA mpya wa Toto Africans ya Mwanza, Khalfan Ngassa ‘Babu’ ameanza vyema baada ya kuiwezesha timu hiyo kuibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya wenyeji Kagera Sugar Uwanja wa Kaitaba, Bukoba katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara leo.
Pongezi kwao wafungaji wa mabao hayo, Jamal Soud dakika ya 47 na Mohamed Soud dakika ya 80, waliomtungua kipa wa zamani wa Simba SC ya Dar es Salaam, Hussein Sharrif ‘Casillas’.
Khalfan Ngassa ‘Babu’ (kushoto) akiwa na mchezaji mwenzake wa zamani wa Pamba na Simba, Juma Amir Maftah
Huo ulikuwa mchezo wa kwanza Toto ikicheza chini ya kocha mpya, Khalfan Ngassa baada ya kuondolewa kwa Rogasian Kaijage aliyekuwa kocha wa timu tangu mwanzo wa msimi baada ya kuondolewa kwa John Tegete.
Kwa matokeo hayo, Toto inafikisha point inane baada ya kucheza mechi nane, huu ukiwa mchezo wa pili kushinda baada ya kufungwa mechi nne na kutoa sare mbili.
0 comments:
Post a Comment