Sturridge |
KLABU ya Manchester City inajiandaa kumsajili Daniel
Sturridge wa Chelsea kwa dau la pauni Milioni 10, ikitumia mwanya wa mchezaji huyo
kuboreka na klabu yake ya sasa.
Inafahamika kwamba Roberto Mancini anataka kumsajili tena mchezaji
huyo aliyekuzwa Man City na kuna imani ataendelea vizuri kisoka akiwa Etihad.
Sturridge amebakiza mwaka mmoja tu katika mkataba wake Chelsea
na anaangalia upya mustakabali wake baada ya kuwa anasugua makalio benchi miezi
ya mwishoni mwa msimu, kiasi cha kukosa nafasi kwenye kikosi cha England cha
Euro 2012.
City inapewa nafasi kubwa ya kuinasa saini ya kinda huyo wa
miaka 22, anahusishwa mno na mpango wa kurejea Manchester na alipigwa picha
hivi karibuni katika mapumziko, akiwa na Micah Richards, visiwa vya Caribbean.
Anaangalia mustakabali wake katika wakati ambao Chelsea inakisuka
upya kikosi chake katika safu ya ushambuliaji, kwa kubeba nyota wapya kama Hulk, Eden Hazard na Marko
Marin, wakati Kevin De Bruyne pia atatua moja kwa moja Stamford Bridge kwa
ajili ya msimu ujao.
Chelsea itataka pauni Milioni 12 kumuachia Sturridge, ambaye
aliwekwa kama mchezaji wa ‘spea’ kwenye kikosi cha England, kufutaia msimu
ambao aliifungia klabu yake mabao 13 na kuichezea mechi mbili timu yake ya
taifa.
Pamoja na hayo, City ilikubaliana na Chelsea kupata asilimia
15 iwapo nyota huyo atauzwa wakati inamuuza mchezaji wake huyo wa zamani wa akademi
yao, kwenda Stamford Bridge mwaka 2009 na kwa sababu hiyo ina matumaini ya
kumsajili kwa pauni Milioni 10 tu.
Vyanzo vimesema kwamba kinda huyo wa miaka 22, mshahara wa
pauni 65,000 kwa wiki anazopewa na Chelsea mchezaji huyo haliwezi kuwa tatizo
kwa City.
Mancini anamzimikia kinoma Sturridge na aliwahi kusema siku
chache baada ya kuanza kazi Etihad kwamba anasikitika kijana huyo kuuzwa
Chelsea.
Sturridge amechanganyikiwa na hafurahii kupangwa pembeni badala
ya nafasi ya mshambuliaji wa kati, jambo ambalo limemponza hadi kupoteza namba
yake katika kikosi cha England.
Baada ya kiwango chake kushuka, akawa anakaa benchi bila
kutumika kabisa katika fainali zote, Ligi ya Mabingwa Ulaya na Kombe la FA.
0 comments:
Post a Comment