• HABARI MPYA

    Friday, April 13, 2012

    POINTI ZA YANGA, DANADANA ZAANZA

    Tibaigana, Mwenyekiti Kamati ya Rufaa
    KIKAO cha cha Kamati ya Nidhamu ya Shirikisho la Soka Tanzania TFF, kilichokuwa kifanyike kesho, kujadili rufani ya Yanga kupinga kunyang’anywa pointi tatu kwa kumchezesha Nadir Haroub ‘Cannavaro’ katika mechi dhidi ya Coastal Union, kimeahirishwa.
    Kamati hiyo chini ya Mwenyekiti wake Kamanda Mstaafu wa Polisi, Kanda Maalum Dar es Salaam, Alfred Tibaigana sasa kitafanyika Jumanne ijayo, (Aprili 17 mwaka huu) saa 9 alasiri kwenye ofisi za TFF.
    Wakati huo huo: Vyama vya mpira wa miguu vya mikoa 17 ya Tanzania Bara vimewasilisha majina ya mabingwa wake kwa ajili ya Ligi ya Taifa iliyopangwa kuanza Aprili 22 mwaka huu katika vituo vitatu.
    Mikoa hiyo na mabingwa wake katika mabano ni Kigoma (Kanembwa FC ya Kibondo), Kilimanjaro (Forest FC ya Siha), Ruvuma (Mighty Elephant ya Songea), Dodoma (CDA), Rukwa, (Mpanda Star ya Mpanda), Iringa (Kurugenzi FC ya Mufindi) na Lindi (Lindi SC).
    Mingine ni Mtwara (Ndanda FC), Shinyanga (Mwadui FC), Mara (Polisi Mara), Singida (Aston Villa), Arusha (Flamingo SC) na Tabora (Majimaji FC). Mikoa ambayo haijawasilisha mabingwa wake ni Manyara, Dar es Salaam, Mwanza, Tanga, Morogoro, Pwani na Kagera.
     
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: POINTI ZA YANGA, DANADANA ZAANZA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top