• HABARI MPYA

    Friday, April 13, 2012

    NI BALAA EL CLASSICO LA GHANA JUMAPILI

    El Classico la Ghana inakuwaga hivi
    WAPINZANI wa jadi katika soka ya Ghana, Asante Kotoko na Hearts of Oak watamenyana Jumapili katika Ligi Kuu ya nchini humo, Uwanja wa Baba Yara, Kumasi.
    Ikijukana kwa jina la ‘El-Classico ya Ghana,’ barabara zote zitaelekea Kumasi; maarufu kama Jiji la Bustani kwa watu wa matawi ya juu.
    Mechi baina ya timu hizo mbili inavutia mno na wapenzi wa soka na huwa kivutio kikubwa inapowadia na wafanyabiashara hunufaika kiuchumi kwa kuuza bidhaa zao uwanajni.
    Kama ilivyo ada Uwanja wa Baba Yara, unatarajiwa kupambwa na rangi nyekundu za Asante Kotoko na njano zenye bluu na nyekundu kidogo za Hearts of Oak.
    Timu ya Porcupine Warriors inawazidi vigogo hao pointi 10 katika msimamo wa Ligi Kuu.
    Kwa kuzingatia kwamba Hearts of Oak imeshinda mechi tatu zilizopita dhidi ya wapinzani wao hao katika Uwanja huo huo, wenyeji watakuwa chini ya shinikizo hasa ikizingatiwa pia wanawania taji la kwanza la Ligi Kuu tangu 2008.
    Kivutio zaidi ni katika mabenchi ya klabu zote, wote wana makocha ambao ni wachezaji wa zamani wa timu ya taifa ya Ghana, Black Stars.
    Maxwell Konadu yupo klabu yake ya zamani, Asante Kotoko wakati Nahodha wa zamani wa timu ya taifa, Charles Akonnor yuko Hearts of Oak.
    Akonnor ameiongoza Hearts of Oak kushinda mechi zao mbili kati ya tatu zilizopita tangu aanze kazi, lakini amesema mchezo huo umekuja katika wakati mbaya.
    Katika mechi 46 ambazo Asante Kotoko walikuwa wenyeji; wameshinda 16, Hearts of Oak 18 na 12 ziliisha kwa sare.
    Katika mechi nyingine, Ashantigold itasafiri Port City kumenyana na Tema Youth wakati Medeama SC na Bechem United watamenyana Uwanja wa Tarkwa Park.
    Nayo timu ya zamani ya kipa wa Yanga, Yaw Berko, Liberty Professionals itaonyeshana kazi na Hearts of Lions, Aduana Stars na Berekum Arsenals na Dwarfs dhidi ya Wassaman.
    Mabingwa watetezi, Berekum Chelsea wagtacheza na Edubiase FC kwenye Uwanja wa Golden City Park.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: NI BALAA EL CLASSICO LA GHANA JUMAPILI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top