 |
| Wachezaji wa Yanga wakimpongeza Msuva |
 |
| David Luhende akisikitika baada ya kukosa bao la wazi |
 |
| Luhende anatoa krosi |
 |
| Hamisi Kiiza kulia |
 |
| Hatari langoni mwa Lyon |
 |
| Hatari langoni mwa Lyon |
 |
| Luhende akitafuta mbinu za kumtoka mtu |
 |
| Luhende amekwishamtoka mtu anachanga mbuga |
 |
| Kiungo wa Lyon, Adam Kingwande akiondosha mpira miguuni mwa Haruna Niyonzima |
 |
| Niyonzima akilalamika baada ya kudondoshwa |
 |
| Kingwande chini naye |
 |
| Semmy Kessi kushoto amekwishamtupa mtu chini, Msuva kulia na kilichofuata ni penalti |
 |
| Msuva akiinuka baada ya kuangushwa na Kessy |
 |
| 11 wa Yanga walioanza leo |
 |
| 11 wa Lyon walioanza leo |
 |
| Msuva akishangilia bao |
Na
Mahmoud Zubeiry
YANGA SC imeibuka na ushindi wa mabao 4-0 dhidi ya Africfan Lyon, zote
za Dar es Salaam katika mchezo wa kirafiki wa kujipima nguvu uliofanyika Uwanja
wa Taifa, Dar es Salaam.
Yanga ilitumia mchezo huo kuwapima wachezaji wake kabla ya kuanza kwa
Ligi Kuu na haukuwa mwanzo mbaya, timu ikicheza kwa utulivu na hata kuhimili
vishindo vya wapinzani.
Didier Kavumbangu, mshambuliaji mpya wa klabu hiyo aliyesajiliwa
kutoka Atletico Olympique ya Burundi, alikuwa wa kwanza kuwainua vitini
mashabiki wa Yanga dakika ya sita baada ya kupiga mpira ambao beki alipojaribu kuokoa ulimgonga kipa wake na kuingia nyavuni.
Hadi mapumziko, Yanga walikuwa mbele kwa bao hilo 1-0 na kipindi cha
pili, Haruna Niyonzima aliifungia Yanga bao la pili kwa penalti dakika ya 57, baada
ya Simon Msuva kuchezewa rafu na Semmy Kessy kwenye eneo la hatari.
Frank Damayo aliyeingia kuchukua nafasi ya Athumani Iddi ‘Chuji’
kipindi cha pili alitoa pasi nzuri kwa Simon Msuva ambaye aliifungia Yanga bao
la tatu dakika ya 72, kabla ya Jerry Tegete kufunga la nne dakika ya 90+1.
Baada ya mchezo huu, Yanga ambao ni mabingwa wa Afrika Mashariki na Kati,
Kombe la Kagame inatarajiwa kuondoka Dar es Salaam Jumatano kwenda Kigali, Rwanda
ambako itaweka kambi ya wiki mbili kujiandaa na Ligi Kuu.
Ikiwa huko, Yanga itacheza mechi kadhaa za kujipima nguvu na vigogo wa
Rwanda, kama APR, Rayon, Atracao na Polisi kabla ya kurejea Dar ves Salaam
kuanza maandalizi ya Ligi Kuu.
0 comments:
Post a Comment