![]() |
| Kikosi cha Yanga na Kombe la Kagame |
Na Prince Akbar
RAIS wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, Jakata Mrisho Kikwete amewapa mwaliko mabingwa wa Afrika
Mashariki na Kati mara mbili mfululizo, Yanga SC kupeleka Kombe lao Ikulu.
![]() |
| Rais Kikwete |
Mwenyekiti wa klabu ya
Yanga ya Dar es Salaam, Yussuf Mehboob Manji amesema kwamba wanashukuru kwa
mwaliko huo na watakwenda huko, wakirejea kutoka Rwanda ambako kikosi chao
kinakwenda jioni hii.
Manji pia alisema
wanatarajia kufungua tawi la klabu yao nchini Rwanda, kufuatia uhusiano mzuri
uliopo, baina ya klabu hiyo na nchi hiyo kwa pamoja na rais wake, Paul Kagame.
Manji alisema hayo
wakati akizungumza na Waandishi wa Habari leo, makao makuu ya klabu makutano ya
mitaa ta Twiga na Jangwani, Dar es Salaam kuhusu mwaliko wa mabingwa hao Klabu
Bingwa Afrika Mashariki na Kati, Kombe la Kagame kutoka kwa rais wa Rwanda,
Kagame.
| Manji akizungumza na wachezaji wa Yanga |
“Tunategemea kufungua
tawi jipya la Yanga nchini Rwanda, hiyo itasaidia kuongeza wanachama nje ya
nchi kwa kuanzia na Rwanda,”alisema Ofisa huyo Mtendaji Mkuu wa Quality Group Limited.
Yanga itakua Rwanda kwa
wiki moja kujiandaa na msimu mpya wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara na
wakiwa watacheza mechi tatu za kirafiki dhidi ya Rayon Sports, Polisi na APR.
Kuhusu mchezaji mpya
aliyesajiliwa kutoka FC Lupopo ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) na APR
ya Rwanda, Mbuyu Twite, Manji alisema ataungana
na wenzake nchini Rwanda na mara baada ya kambi hiyo ya wiki moja atarudi na
timu kuja kuanza kuitumikia katika msimu mpya w aligi kuu.
Yanga inakwenda Rwanda
na msafara wa watu 42, wakiwemo wachezaji 29, Maofisa watano wa benchi la
Ufundi na viongozi wanane.
Viongozi wanaondoka na
timu ni Mwenyekiti Yussuf Manji, Makamu Mwenyekiti, Clement Sanga na Wajumbe wa
Bodi ya Wadhamini Mama Fatma Karume, Francis Kifukwe na Seif Ahmed ‘Magari’
sambamba na Wajumbe wa Kamati ya Utendaji, Abdallah Bin-Kleb na Salum Rupia.
Benchi
la ufundi ni kocha mkuu; Tom Saintfiet, Kocha Msaidizi Fred Felix Minziro, Meneja
Hafidh Saleh, Daktari, Sufiani Juma na Mtunza vifaa Mahmoud Omary ‘Mpogolo’,
wakati wachezaji ni makipa: Yaw Berko, Ally Mustafa ‘Barthez’ na Said Mohamed.
Mabeki Shadrack Nsajigwa, Godfrey Taita, Juma Abdul, Oscar Joshua, Stefano Mwasyika,
David Luhende, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Kelvin Yondan, Ibrahim Job, Ladisalus
Mbogo; viungo Athumani Iddi ‘Chuji’, Juma Seif ‘Kijiko’, Salum Telela, Simon
Msuva, Shamte Ally, Omega Seme, Idrisa Rashid, Nizar Khalfan, Haruna Niyonzima,
Frank Domayo, Rashid Gumbo, Nurdin Bakari na washambuliaji; Said Bahanunzi ‘Spider
Man’, Hamis Kiiza ‘Diego’, Jerry Tegete na Didier Kavumbangu.




.png)
0 comments:
Post a Comment