![]() |
| Simba na Azam walivyokutana mara ya mwisho Kombe la Kagame |
Na Mahmoud Zubeiry
MECHI ya Ngao ya Jamii
ya kuashiria kufunguliwa kwa pazia la Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara,
inatarajiwa kuchezwa Septemba 8, mwaka huu, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam,
ikizikutanisha bingwa wa ligi hiyo, Simba SC na washindi wa pili, Azam FC.
Habari za ndani kutoka
Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), zimesema kwamba, kuchelewa kwa mechi hiyo ambako
kumeenda sambamba na kuchelewa kuanza kwa ligi hiyo, kumetokana na kuchelewa
kufikiwa mwafaka mapema wa mkataba mpya wa udhamini wa Ligi Kuu.
Mkataba wa awali wa
Vodacom na TFF unafikia tamati mwishoni mwa mwezi huu na kusainiwa mkataba
mwingine, baada ya majadiliano yanayoendelea.
Lakini kwa kuwa Mkutano
Mkuu wa TFF uliopita uliridhia kuanzia msimu ujao Ligi Kuu iendeshwe na kampuni
itakayoundwa na klabu za Ligi Kuu mjadala kuhusu udhamini mpya wa ligi umekuwa
mrefu kutokana na kuhusisha pande tatu, klabu, wadhamini na shirikisho.
Lakini sasa, kwa
vyovyote, hata maridhiano ya mkataba mpya wa udhamini na Vodacom yachelewe
tena, mechi hiyo itachezwa Septemba 8, ikiwa ni wiki moja kabla ya kuanza kwa
Ligi Kuu.
Kihistoria hiyo itakuwa
mechi ya tano ya Ngao ya Jamii kuchezwa nchini na ya pili kuishirikisha timu nje
ya wapinzani wa jadi wa soka ya Tanzania, Simba na Yanga.
Mtibwa ilicheza na
Yanga mwaka 2009, baada ya Simba kugoma na ikashinda mabao 2-1 na kutwaa Ngao,
wakati kabla ya hapo, mwaka 2001, Ligi Kuu ya Tanzania ikiwa bado inadhaminiwa
na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), kupitia bia ya Safari Lager, ilichezwa mechi
ya kwanza ya Ngao kihistoria.
Katika mechi hiyo,
Yanga ilishinda mabao 2-1 dhidi ya Simba na mwaka juzi Yanga iliifunga tena
Simba kwa penali 3-1 kufuatia sare ya 0-0 na mwaka jana, Simba ilitwaa Ngao ya
kwanza katika historia yake, kwa kuifunga Yanga mabao 2-0.
MABINGWA
WA MECHI ZA NGAO YA JAMII:
Mwaka Mshindi Matokeo
2001 Yanga 2-1 Simba
2010 Yanga
0-0 Simba (3-1penalti)
2011 Simba
2-0 Yanga



.png)
0 comments:
Post a Comment