• HABARI MPYA

    Friday, August 31, 2012

    MTIBWA YASAJILI MGANDA, ITC YATUMWA FASTA

    Kocha wa Mtibwa, Mecky Mexime

    Na Prince Akbar
    SHIRIKISHO la Soka Uganda (FUFA) limetuma Hati ya Uhamisho wa Kimataifa (ITC) kwa ajili ya mchezaji Ayoub Hassan Isiko aliyejiunga na Mtibwa Sugar akitokea timu ya Bull FC ya nchini humo.
    ITC hiyo ilitumwa jana (Agosti 30 mwaka huu), hivyo kufanya wachezaji ambao ITC hazijapatikana hadi sasa kubaki wawili tu. Dirisha la usajili wa wachezaji litafungwa rasmi Septemba 4 mwaka huu.
    Wachezaji ambao ITC zao bado hazijapatikana ni Salum Kinje na Pascal Ochieng kutoka AFC Leopards ya Kenya waliojiunga na Simba. ITC hizo zinatarajiwa kupatikana wakati wowote kwani tayari Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limeshaziomba kwa Shirikisho la Mpira wa Miguu Kenya (FKF) baada ya nyaraka zote zilizokuwa zikitakiwa kupatikana.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MTIBWA YASAJILI MGANDA, ITC YATUMWA FASTA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top