Robin van Persie ataongezewa pauni Milioni 10 zaidi katika mshara wake wa pauni 250,000 kwa wiki Manchester United - kama atadumu katika klabu hiyo kumalizia mkataba wake wa miaka minne.
Malipo hayo yatakayoongezwa kwa mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Uholanzi aliyezaliwa miaka 29 iliyopita, kwa kuishi kwake Old Trafford ndani ya mkataba wake wote wa miaka minne, ni nje ya posho ambazo atashinda mataji ya United kama Ligi Kuu, Kombe la FA, Kombe la Ligi na Ligi ya Mabingwa
Wengi ndani ya United, akiwemo Mtendaji Mkuu, David Gill, waliulizwa iwapo uwekezaji wa pauni milioni 64 kwa Van Persie - pamoja na uhamisho wa pauni Milioni 24 kwa mkataba wa miaka minne kama utalipa.
MKWANJA ZAIDI: Van Persie ataingiza pauni Milioni 10 zaidi akidumu Old Trafford
SOURCE: http://www.dailymail.co.uk


.png)
0 comments:
Post a Comment