• HABARI MPYA

    Sunday, August 19, 2012

    AKINA BANKA WAZIDI KUTAKATA KENYA

    BANDARI ya Mombasa, Kenya inayopigwa tafu na wachezaji wanne wa Kitanzania, David Naftali (pichani), Meshack Abel, Mohamed Banka na Thomas Maurice, imeendelea kujiimarisha katika harakati za kurejea Ligi Kuu ya Kenya, baada ya leo kuifunga mabao 3-1 Iron Strikers.
    Mabao ya Bandari ambayo msimu huu imempoteza kipa Mtanzania, Ivo Mapunda aliyehamia Gor Mahia, yalifungwa na Erick Okoth, kiungo wa zamani wa Azam FC, Crispin Odula na mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Tomas Maurice, kwa mpira wa adhabu.
    Maurice, ambaye pia amewahi kuchezea Mtibwa Sugar, ndiye alikuwa nyota wa mchezo wa leo, kwa mujibu wa beki wa Bandari, Naftali aliyewahi kuchezea Simba SC.
    Ushindi huo, unaifanya Bandari iliyoshuka Daraja msimu uliopita, kuendelea kuongoza Ligi Daraja la Kwanza Kenya, baada ya kufikisha pointi 57, ikifuatiwa na Sharks Kariobang, yenye pointi 48, ambayo leo imetoka sare na timu ya zamani ya mshambuliaji wa AJ Auxerre ya Ufaransa, Dennis Oliech, Mathare United.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: AKINA BANKA WAZIDI KUTAKATA KENYA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top