Baada ya sala ya Eid
El Fitri, kwa pamoja na familia yangu, tulikwenda kujumuika na watoto (yatima)
wa kituo cha New Home Family Group, kilichopo Mji Mwema Ungondoni, Kigamboni,
Dar es Salaam.
Tulikula pamoja,
tukafurahia Eid yetu. Kwangu, kama mzazi nilifarajika kuwapa faraja watoto wa
kituo hicho. Nilifarijika kuwapa watoto wangu somo fulani, katika umri mdogo.
Nilifurahi jinsi walivyoonyesha upendo kwa watoto wenzao. Nilifurahi jinsi
walivyoonyeshwa upendo na watoto wa kituo hicho.
Mwanzoni, walikuwa kama
waoga waoga, kwa sababu ni mara ya kwanza kwao kwenda kujumuika na watoto ambao
hawafahamiani nao. Lakini kadiri walivyozidi kukaa pamoja, walizoeana na hata
niliposema sasa inatosha tuondoke, nilihisi kama nawakatili.
Watoto wangu na watoto
wa kituo hicho walipenda kuendelea kuwa pamoja. Watoto wangu, wakaomba siku
moja niwapeleke tena kwenye kituo hicho wakacheze na wenzao. Wote walipata
marafiki.
Kwa ujumla nilifurahi
sana kutembelea kituo hicho chenye jumla ya watoto 35, ambacho bado kinahitaji
misaada ili kiweze kuwahudumia vema watoto hao, kama ambavyo mmoja wa walimu wa
kituo hicho, Michael Lugendo, alisema kwamba kwa sasa wanakabiliwa na
changamoto ya choo.
Choo chao ‘kimefurika’
kwa sababu kilitengenezwa vibaya na wanahitaji misaada ya fedha au vifaa vya
ujenzi, ili wawewze kukikarabati kiwe katika hali nzuri na kuepuka kuhatarisha
afya za watoto zaidi ya 35.
Sote tunafahamu,
chanzo kikubwa cha maradhi ya milipuko ni ukosefu wa choo bora- basi ipo haja
kwa wenye uwezo kujitolea kusaidia changamoto hiyo inayowakabili watoto wetu wa
New Hope Family Centre, Mji Mwema Ungondoni, Kigamboni.
Naam, kwangu, mimi
mtoto wa marehemu Alhaj Ramadhan Zubeiry, hivi ndivyo nilivyosherehekea Eid
yangu na sasa maisha mengine yanaendelea kama kawaida. Eid Mubbarak.
| Watoto wakipakuliwa chakula |
Princess Asia akiwa na
rafiki yake wa kituo hicho
|
Prince Akbar akiwa na
rafiki yake wa kituo hicho
|
Precious akiwa na
rafiki yake wa kituo hicho
|
Prince Akbar wa pili
kutoka kulia, akila na watoto wenzake wali ndondo
|
Princess Asia katikati
kutoka, akila na watoto wenzake wali ndondo.
|
Precious kushoto,
akiwa na Princess Asia na mtoto wa kituo hicho wakipata wali ndondo
|
| Prince Akbar mwenye kanzu |
Katika picha ya
pamoja, mimi na watoto wa kituo hicho
|
Mtoto Precious
akikabidhi zawadi aliyowapelekea watoto wa kituo hicho kwa Bi Maimuna Mussa,
mmoja wa walezi wa kituo hicho.
|
Mtoto Princess Asia,
akikabidhi zawadi aliyowapelekea watoto wa kituo hicho kwa Bi Maimuna Mussa
|
Mtoto Prince Akbar
akikabidhi zawadi aliyowapelekea watoto wa kituo hicho kwa Bi Maimuna Mussa
|
Prince Akbar
akikabidhi zawadi zaidi kwa mtoto mwenzake.
|
Nikiwa na Michael
Lugendo, ninawa tayari kwa chakula
|
Nikiwa na Michael
Lugendo, tukipata chakula, huku tukijadiliana mambo
|
Nikiwa na Michael
Lugendo, tukipata chakula, huku tukijadiliana mambo
|
Nikiwa na Michael
Lugendo, tukipata chakula, huku tukijadiliana mambo
|
Nikiwa na Michael
Lugendo, tukipata chakula, huku tukijadiliana mambo
|
Nikiwa na Michael
Lugendo, tukipata chakula, huku tukijadiliana mambo
|
Nikiwa na Michael
Lugendo, tukipata chakula, huku tukijadiliana mambo
|
Nikiwa na Michael
Lugendo, tukipata chakula, huku tukijadiliana mambo
|


.png)
0 comments:
Post a Comment