| JEMBE TUTALIKOSA LEO; Bahanuzi 'Spider Man' kushoto akiwatoka mabeki wawili wa APR, kulia ni Twite wakati bado yupo APR. |
Na Mahmoud Zubeiry
MFUNGAJI bora wa
Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, Said Bahanuzi ‘Spider Man’ hatacheza leo
mechi ya kirafiki dhidi ya African Lyon kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam
kutokana na maumivu ya goti.
Meneja wa Yanga,
Hafidh Suleiman ameiambia BIN ZUBEIRY leo kwamba, Bahanuzi
anasumbuliwa na maumivu ya goti na leo atamuona daktari wa klabu, Dk Sufiani
Juma kwa ajili ya uchunguzi zaidi.
Yanga SC leo
wanatarajiwa kushuka dimbani kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, kumenyana
na African Lyon katika mchezo wa kirafiki, ambao imeelezwa beki Mbuyu Twite
kutoka APR ya Rwanda atacheza.
Lakini mbaya zaidi
hadi asubuhi hii, beki huyo alikuwa hajawasili nchini, ingawa BIN
ZUBEIRY ilipowasiliana na kiongozi mmoja wa klabu hiyo, alisema ‘Shaka
ondoa, utamuona Twite uwanjani leo’.
Huo utakuwa mchezo
wa kwanza wa kirafiki kwa Yanga, tangu itwae ubingwa wa Kombe la Kagame mwezi
uliopita na kwa wakati huo imekuwa ikijifua tu kwenye Uwanja wa sekondari ya Loyola,
Mabibo, Dar es Salaam.
Mbali na Twite,
mashabiki wa Yanga leo pia watapata fursa ya kumshuhudia kwa mara ya kwanza,
mshambuliaji Didier Kavumbangu waliyemsajili kutoka Atletico Olimpique ya
Burundi.
Kavumbangu ndiye
aliyewafunga Yanga mabao yote mawili, walipomenyana na timu hiyo ya Burundi na
kulala 2-0 na kwa kuwa mfungaji bora wa Kagame, Said Bahanuzi ‘Spider Man’ ni
mgonjwa, Didier lazima ataanza.
Tayari Yanga imewasilisha
usajili wake Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), hivyo kocha Tom Saintfiet raia wa
Ubelgiji anaweza kumpanga yeyote atakaye.
Kikosi kamili cha
Yanga ni; Makipa; Yaw Berko, Ally Mustafa ‘Barthez’ na Said
Mohamed.
Mabeki; Shadrack Nsajigwa (Nahodha), Godfrey Taita, Juma Abdul, Oscar
Joshua, David Luhende na Stephano Mwasika, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Kevin
Yondan, Mbuyu Twite, Ibrahim Job na Ladislaus Mbogo.
Viungo; Athuman Idd ‘Chuji’, Juma Seif ‘Kijiko’ na Salum Telela, Nizar
Khalfan, Shamte Ally, Idrisa Rashid, Omega Seme, Haruna Niyonzima, Rashid Gumbo
na Nurdin Bakari.
Washambuliaji; Said Bhanaunzi ‘Spider Man’, Hamisi Kiiza ‘Diego’, Didier
Kavambagu na Jerry Tegete.
Kiungo
Frank Domayo na mshambuliaji Simon Msuva, wanaendelea kukomazwa katika kikosi
cha kwanza, wakitokea kikosi cha pili. Awali Yanga ilikuwa icheze na Coastal
Union, lakini mechi hiyo imefutwa.


.png)
0 comments:
Post a Comment