Manji; Mwenyekiti mpya mtarajiwa Yanga |
YUSSUF Mehboob Manji ni miongoni mwa wanachama 29 wa Yanga
waliorudisha fomu leo kwa ajili ya kuwania nafasi mbalimbali za uongozi katika
klabu hiyo, katika uchaguzi uliopangwa kufanyika Julai 15, mwaka huu, Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa Kamati ya Uchaguzi ya Yanga, Francis
Kaswahili amesema jioni hii katika Mkutano na Waandishi wa Habari kwamba, Manji
ni miongoni mwa wanachama wanne waliorudisha fomu kwa nafasi ya Mwenyekiti,
wengine wakiwa ni John Jambele, Edgar Chibura na Sarah Ramadhani.
Katika nafasi ya Makamu Mwenyekiti, Kaswahili aliyekuwa
akizungumza mbele ya mwakilishi wa kamati ya Uchaguzi ya Shirikisho la Soka
Tanzania (TFF), Hassan Chabanga Dyamwale alisema wamerudisha wanachama watano
ambao ni Ally Mayay, Ayoub Nyenzi, Yono Kevela na Clement Sanga.
Katika nafasi za Ujumbe waliorudisha ni Lameck Nyambaya,
Ramadhani Mzimba ‘Kampira’, Mohamed Mbaraka, Ramadhani Said, Edgar Fongo, Beda
Simba, Ahmad Gao, Mussa Katabaro, George Manyama, Aaron Nyanda, Abdallah Bin
Kleb, Omary Ndula, Shaaban Katwila, Jumanne Mohamed Mwammenywa, Abdallah
Mbaraka, Peter Haule, Justin Baruti na Abdallah Sharia.
Kaswahili alisema Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Muhingo
Rweyemamu, Mfanyabiashara Muzamil Katunzi na Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini,
Eliakhim Masu hawakurudisha fomu, wakati Isaac Chanzi pia hakurudisha fomu ya
Makamu Mwenyekiti.
Mzee Dyamwale kulia akifafanua jambo kwa Waandishi kumsaidia Kaswahili, kushoto |
Manji alimchukulia fomu Bin Kleb, ambaye naye leo amemrejeshea
fomu Yussuf, akisindikizwa na Seif Ahmad ‘Magari’.
0 comments:
Post a Comment